NA MWANDISHI WETU, MTWARA
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Bw.
Bernard Konga amesema kuwa utaratibu wa vifurushi vya bima ya afya hauondoi
taratibu mbalimbali zilizowekwa na serikali za kugharamikia matibabu kwa watu
wasiojiweza ikiwemo wazee.
Bw. Konga amesema hayo leo Mkoani Mtwara wakati wa Mkutano
na wanachama wa Chama wa Waandishi wa Habari wa Mikoa ya Lindi na Mtwara walimpotaka
atolee ufafanuzi wa kwanini gharama za
matibabu kwa wazee katika vifurushi vipya vya bima ya afya ni tofauti na
makundi mengine.
“Utaratibu unasema hivyo, hata Sera ya Afya ya Mwaka 2007
ukurasa ya 29 inasema serikali inatambua
uwepo wa watu wasio na uwezo kutoka makundi ya, watoto, wazee na kina mama
wajawazito, utaratibu huu unalenga wazee wenye uwezo na hauondoi taratibu za serikali
za kugharamia makundi hayo ndio maana utaratibu wa msamaha kwa makundi hayo
bado upo na unaendelea kama kawaida.
Aidha Bw. Konga amesema kuwa viwango vyake ni tofauti
kutokana na hali halisi kuwa kadiri umri unavyokwenda mahudhurio ya hospitalini
yanaongezeka na uhalisi wa gharama za matibabu zinakuwa kubwa zaidi.
“Utaratibu huu hauangalii uwezo wa kulipia fedha. bali
unaangalia uhalisi wa gharama za matitabu, matatizo ya figo, matatizo na moyo
mara nyingi yanakuwa kwa watu wenye umri kuanzia miaka hamsini na kuendelea, leo
hii ugonjwa mfano wa tezi dume, gharama zake ni kubwa sana”-Bw. Konga
Akiongea wakati wa kuwasilisha mada kwa wanahabari hao
Meneja Masoko na Huduma kwa Wateja Bw. Hipoliti Lello amesema kuwa Serikali
imedhamiria kuhakikisha kila mtanzania anajiunga na bima ya afya na ndio maana
mfuko umekuja na utaratibu wa vifurushi vyenye gharama kuanzia Laki moja na
Tisini na Mbili.
“Awali tulikuwa na utatibu wa Milioni Moja na Nusu kujiunga
kwa mtu mmoja lakini ilikuwa ni changamoto kubwa kwa mtu mmoja mmoja na ndio maana
tumeishusha hadi kufikia laki moja na tisini na mbili, hii yote ni dhamira ya
dhati ya kuhakikisha tunamrahisishia Mtanzania kujiunga na bima ya afya”-Bw.
Lello.
Naye Mkurugenzi wa Huduma za Uanachama wa Mfuko wa Taifa ya
Bima ya Afya Bw. Christopher Mapunda amesema kuwa tangu kuanza kwa vifurushi
hivi muitikio wa watanzania umekuwa ni mkubwa hasa baada ya kupunguzwa kwa bei
na hii imeonyesha kuwa huduma za bima za afya zilikuwa na uhitaji mkubwa
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Bw.
Bernard Konga akiongea na wanachama wa Chama wa Waandishi wa Habari wa Mkoa wa
Mtwara na Lindi kuwaelimisha kuhusu mpango wa Mfuko huu kuwafikia wananchi
wengi zaidi kupitia makundi maalum na Vifurushi vya Bima ya Afya, leo
18.12.2019 Mkoani Mtwara
Meneja Masoko na Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa Taifa
ya Bima ya Afya Bw. Hipoliti Lello
akiwasilisha mada kwa wanahabari wa Mikoa ya Lindi na Mtwara kuhusu mpango wa
Mfuko huu kuwafikia wananchi wengi zaidi kupitia makundi maalum na Vifurushi
vya Bima ya Afya, leo 18.12.2019 Mkoani Mtwara
Wanahabari wa Mikoa ya Lindi na Mtwara wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya
Afya Bw. Bernard Konga wakati wa mkutano na wataalam wa Mfuko wa Taifa wa Bima
ya Afya kuhusu mpango wa Mfuko huu kuwafikia wananchi wengi zaidi kupitia
makundi maalum.
Wanahabari wa
Mikoa ya Lindi na Mtwara wakifuatilia uwasilishaji wa mada wakati wa mkutano na
wataalam wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kuhusu mpango wa Mfuko huu kuwafikia
wananchi wengi zaidi kupitia makundi maalum na Vifurushi vya Bima ya Afya, leo
18.12.2019 Mkoani Mtwara
PICHA NA IDARA YA
HABARI-MAELEZO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...