MWENYE njaa usimpe samaki mpe ndoano ili aweze kuvua samaki wengine ili akila apate nguvu na kwenda kuvua samaki wengi zaidi.

Kauli hiyo ameitoa Katibu Mkuu Sayansi wa wizara ya elimu Sayansi na Teknolojia, Dkt.James Mdoe wakati akifunga mafunzo ya washindi wa shindano la kitaifa la Sayansi na Teknolojia jijini Dar es Salaam leo, Amesema kuwa  sio utaratiu wa serikali kugawa fedha kwa wabunifu bali serikali inajukumu la kuwajengea uwezo ili waweze kumiliki bunifu zao kisheria ili mtu mwinvgine asije kujitokeza kufanya kitu alicho kibuni mtu mwingine.

Dkt. Mdoe amesema kuwa wabunifu wengi kuwaendeleza haina maana kuwa tuwape pesa, ni kitendo cha kuwajengea uwezo ili waweze kuendeleza ubunifu ule kwani ni wa mbunifu mwenyewe.

"Sasa jukumu letu kam serikali ni kuwezesha ili uweze kutoka hatua moja kwenda nafasi bora zaidi ili uunifu ule uweze kusaidia zaidi" Amesem Dkt. Mdoe.

Amesema kuwa kunavitu amavyo mbunifu anahitaji ili aweze kuendeleza ubunifu wake  na kuwe na mwekezaji  ambaye atachukuwa ubunifu wa mbunifu na kufanya kuwa kitu kikubwa na kuwekeza ili biashara iweze kufanyika.

MAfunzo hayo kwa wabunifu wa shindano la MAKSATU yametolewa na Baraza la uwezeshaji uchumi taifa la Sayansi na Teknolojia, Brela, SIDO, TBS na Cosota ambayo yalitolewa kwa siku nnne kwajili ya kuwajengea uwezo  na kuonesha fursa mbalimali zilizopo.

Amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha miongozo ya kibunifu, maombi mbalimbali ya ubunifu, ili tuweze kupata wabunifu wengi zaidi kwaajili ya manufaa ya nchi ya sasa na ya baadae.

Kwa upande wa wabunifu, Halima Mpita, amesema kuwa yale yote yaliyoanzishwa na wabunifu lazima yatekelezeke kwaaajili ya kuisaidia jamii yetu, katika mahali wanapoelekea wabunifu hao.

"Safari yetu ya MAKSATU ilianzia  aada ya serikali kupitia wizara ya elimu kuundua vipaji 337 na katika kupitia hilo ziliunganishwa na DSI, VETA, COSTECH, DIT,wote hawa walifanya kazi ya pamoja katika kutafuta wabunifu hawa na hatimaye kukawa na mashindano ambayo yalianza machi mwaka huu ndiyo yaliyotupelekea kuwepo hapa leo". Amsema Halima.




Katibu Mkuu Sayansi wa wizara ya elimu Sayansi na Teknolojia,Dkt.James Mdoe akizungumza na washindi wa shindano la kitaifa la ubunifu wa Sayansi na Teknolojia (2019) (MAKSATU) jijini Dar es Salaam leo wakati wa kufunga mafunzo ya siku nne kwa wabunifu hao.
 Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia(COSTECH)Dkt. Amos Nungu akizungumza wakati wa kufunga mafunzo kwa washindi wa shindano la kitaifa la ubunifu wa Sayansi na Teknolojia jijini Dar es Salaam leo.

Mbunifu wa mkaa mbadala, Halima Mpita Akizungumza kwa niaba ya wabunifu wengine na  kutoa shukurani kwa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH),jijini Dar es Salaam leo wakati wa kufunga mafunzo kwa wabunifu walioshinda katika shindano la kitaifa la Ubunifu wa Sayansi na Teknolojia

 Baadhi ya wabunifu wakimsikiliza mgeni rasmi Katibu Mkuu Sayansi wa wizara ya elimu Sayansi na Teknolojia,Dkt.James Mdoe wakati wa kufunga mafunzo ya siku nne kwa waunifu wa shindano la  MAKSATU jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...