Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Mhe. Anne Makinda akiongea wakati wa
uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya
bima ya afya Mkoani Mwanza, ambapo alisema mpango wa vifurushi umekuja
kwa ajili ya kuwajumuisha watanzania wote.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Mhe. Anne Makinda akitoa kadi za bima
za afya kwa wanachama waliojiunga kwa mpango wa vifurushi, leo Mkoani
Mwanza.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Mhe. Anne Makinda akiwa katika picha
ya pamoja wanachama waliojiunga kwa mpango wa vifurushi, leo Mkoani
Mwanza.
Makamu Mwenyekiti wa Machinga Mkoa
wa Mwanza Bw. Joseph Samwel akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni ya
kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya bima ya afya Mkoani
Mwanza, ambapo alisema suala la vifurushi limekuwa kuwa mkombozi kwa
machinga.
Makamu Mwenyekiti wa Bodaboda Mkoa
wa Mwanza Bw. Gerald Nyerembe akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni
ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya bima ya afya Mkoani
Mwanza, ambapo alisema wamelipokea vyema suala la vifurushi vya Bima ya
Afya kwani ni muhimu kwa afya zao.PICHA NA IDARA YA HABARI-MAELEZO
…………………..
Na Mwandishi Wetu.
Jumuiya za Wajasiriamali
wadogowadogo na Waendesha Bodaboda nchini wamepongeza hatua ya
kuanzishwa kwa vifurushi vya bima ya afya ambavyo vimewawezesha katika
kupata matibabu ya uhakika pindi wanapoumwa.
Wakiongea wakati wa uzinduzi
wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya Bima ya
Afya viongozi wa jumuiya hizo wamesema ilikuwa ni hitaji lao la muda
mrefu la kuhakikisha wanachama wao wanakuwa na uhakika wa matibabu kwa
kuwa na bima za afya.
“Tunamshukuru sana Mhe. Rais
Magufuli na serikali ya awamu ya tano kwa kuwa na maono ya kuhakikisha
machinga nasisi tunakuwa na uhakika wa matibabu, awali ilikuwa ni ngumu
sana unaenda hospitali ukiwa na hofu ya gharama lakini kwa sasa
tunatembea kifua mbele, tunapata tiba popote nchini kwa vifurushi
hivi”-Stephen Lusinde Mwenyekiti wa Machinga Taifa
Naye Mwenyekiti wa Bodaboda
Taifa Bw. Michael Haule amesema kuwa ujio wa mpango huu wa vifurushi ni
uthibitisho kwamba serikali ya awamu ya tano kila mtu ni sawa na ndio
maana wao kama bodaboda sasa wamewekewa utaratibu rahisi wa kujiunga na
vifurushi vya bima ya afya kwa gharama nafuu kabisa.
“Zamani ilikuwa ni ngumu sana
kumkuta bodaboda anamiliki kadi ya bima ya afya, bodaboda wengi
wawepoteza maisha kutokana na kukosa huduma bora za matibabu kutoka na
ajali, ila kwasasa suala hilo ni historia, bodaboda sasa ni kama wafalme
tunajidai na kadi zetu”- Michael.
Mwenyekiti wa Bodaboda Mkoa
wa Mwanza Bw. Gerald Nyerembe alisema kuwa wamelipokea suala la
vifurushi kwa kuwa ni muhimu kwa afya zao na wanafarijika sana kwa
Serikali kuwatambua kwani bima imekuwa na faida kubwa kwao.
Aidha, Mwenyekiti wa Machinga
Mkoa wa Mwanza Bw. Joseph Samwel amesema suala la vifurushi limekuja
kuwa mkombozi na kuokoa maisha ya wajasiriamali wadogo kwani bila afya
hakuna maendeleo hivyo wajasiriamali hawana budi kuliona suala la
vifurushi kama mkombozi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...