Kocha wa Yanga Luc Eymael amepewa onyo Kali kwa matamshi aliyoyatoa kuhusu ubaguzi wa rangi katika mchezo dhidi ya Azam FC uliopigwa Januari 18, 2020 na kushuhudia mchezo huyo ukimalizika kwa Yanga kufungwa goli 1-0.

Maamuzi hayo yametolewa na kamati ya Uendeshaji wa Ligi (Kamati ya Saa 72) leo katika ofisi za TFF Jijini Dar es Salaam.

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imempa onyo Kocha wa Klabu ya Yanga, Luc Eymael kwa kufanya vitendo na kutoa matamshi yasiyofaa.

Aidha kamati hiyo imeitaka klabu ya Yanga kutoa tamko juu ya kauli hizo pamoja na vitendo vingine alivyoeleza kuwa siyo vya kiungwana.

Katika adhabu nyingine, Klabu ya Tanzania Prisons na Yanga zimepigwa faini ya Tsh. 500,000 kila mmoja kwa kutokuwakilisha Vikosi vya Timu kwenye kikao cha maandalizi katika mchezo wao wa Desemba 29, 2019

Klabu ya Yanga imetozwa faini ya Tsh. 500,000 kutokana na Washabiki wake kurusha chupa za maji kuelekea uwanjani na wakati wa mapumziko waliwarushia chupa za maji Waamuzi

Vile vile katika mchezo huo Klabu ya Yanga imepigwa faini ya Tsh. 200,000 kwa kutokutumia Chumba Rasmi kilichoandaliwa kwa kubadilishia nguo

Aidha, Wachezaji wa Mbeya City (Kelvin John na Majaliwa Shaban) na Yanga (Mrisho Ngasa, Ramadhani Kabwili na Cleafas Sospeter) kila mmoja amefungiwa michezo mitatu na kupigwa faini ya Tsh. 500,000 kila mmoja kwa kugoma kuingia vyumbani

Kamati imeeleza kuwa katika adhabu za wachezaji waliofungiwa hususani wa Yanga watatumika katika mchezo wa leo mpaka pale Klabu zao watapopata barua kutoka Bodi ya Lig

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...