Katibu Tawala Wilaya ya Kusini Unguja Kibibi Mwinyi akizungumza na
Wananchi wa Paje kuhusu kutoa mashirikiano kwa Madaktari wa Shirika la
utoaji wa Miwani la Sweden wakati akizindua huduma za macho huko Kituo
cha Afya Paje Mkoa wa Kusini Unguja.
Mkuu wa Kitengo kutoka Shirika la utoaji Miwani la Sweden Caroline
Schiller akifanya zoezi la kumpima Macho Mtoto Kassim Juma katika Kituo
cha Afya Paje.
Mmoja kati ya Wananchi waliyojitokeza kupata huduma za macho Maua
Sleiman Said akijaribu kusoma wakati akipatiwa huduma hiyo na Daktari
kutoka Shirika la utoaji wa miwani la Sweden Julia Sandberg katika Kituo
cha Afya Paje Wilaya ya Kusini.
Daktari kutoka Shirika la utoaji wa Miwani la Sweden Emma Elmebno
akimpima Miwani Sofia Khamiss Juma katika hafla iliyofanyika Kituo cha
Afya Paje.
Mratibu kutoka Shirika la utoaji Miwani la Sweden Happiness Urassa
akitoa Maelezo kuhusu zoezi zima la kutoa huduma za macho huko Kituo cha
Afya Paje.
Baadhi ya Wananchi waliofika kupata huduma za macho huko kituo cha Afya Paje Mkoa wa Kusini Unguja. Picha Na Maryam Kidiko - Idara ya habari Maelezo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...