Waziri wa Afya nchini Algeria amethibitisha kwamba nchi hiyo imepokea kisa cha kwanza cha coronavirus katika taarifa iliyotolewa na runinga inayomilikuwa na serikali, ENTV Jumanne jioni.

Waziri Abdel Rahman Ben Bouzid alisema kuwa mgonjwa huyo ni mwanamume raia wa Italia aliyewasili nchini humo Februari 17, kulingana na shirika la habari la Reuters.

Mgonjwa huyo ametengwa kwa sasa.

Algeria imekuwa nchi ya pili Afrika kuthibitisha kupata mgonjwa wa virusi vya Corona.

Misri ilikuwa ya kwanza kuthibitisha kupatika kwa kisa cha virusi vya Corona lakini baadae ikatangaza kwamba mgonjwa huyo hana tena maambukizi na anaendelea kupata nafuu. 
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...