Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na watoto Dk. Zainab Chaula akizungumza na Julieth Mselle Afisa Huduma kwa wateja kutoka MSD wakati alipotembelea katika banda la taasisi hiyo katika Maadhimisho ya Siku ya Madaktari Tanzania ukumbi wa Julius Nyerere Posta. jijini Dar es salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na watoto Dk. Zainab Chaula akimsikiliza Julieth Mselle Afisa Huduma kwa wateja kutoka MSD wakati alipotembelea katika banda la taasisi hiyo katika Maadhimisho ya Siku ya Madaktari Tanzania ukumbi wa Julius Nyerere Posta. jijini Dar es salaam.
Julieth Mselle Afisa Huduma kwa wateja kutoka MSD akitoa maelezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Laurean Bwanakunu wakati alipotembelea katika banda la taasisi yake katika Maadhimisho ya Siku ya Madaktari Tanzania ukumbi wa Julius Nyerere Posta. jijini Dar es salaam
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Laurean Bwanakunu akizungumza na baadhi ya wageni wakati walipotembelea katika banda la taasisi yake katika Maadhimisho ya Siku ya Madaktari Tanzania ukumbi wa Julius Nyerere Posta. jijini Dar es salaam.
Julieth Mselle Afisa Huduma kwa wateja kutoka MSD na Benjamin Massangya afisa Mawasiliano Mwandamizi MSD wakiwa katika banda lao.
...............................................

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na watoto Dk. Zainab Chaula ameiasa Bohari ya Dawa nchini MSD kutotoa dawa bure kwa Hospitali , Vituo vya Afya na Zahanati kote nchini badala yake walipe fedha kama utaratibu unavyotaka na fedha zitakazopatikana kutokana na malipo ya dawa hizo zifanye kazi ya kununua dawa zingine kwa ajii ya kuhudumia watanzania.

Dk. Chaula ameyasema hayo kando ya mkutano wa Maadhimisho ya Siku ya Madaktari Tanzania uliofanyika kwenye ukumbi wa Julius Nyerere Posta jijini Dar es salaam jana wakati alipotembelea banda la MSD ambao walishiriki katika maonesho ya taasisi mbalimbali zinazoshughulikia masuala ya afya.

Dk. Chaula amesema MSD ni wadau muhimu katika afya za watanzania kwani ndiyo wenye wajibu wa kuhakikisha dawa zinapatikana kote nchini na kila wakati kwenye hospitali zetu, Vituo vya Afya na Zahanati hivyo ni muhimu wahakikishe fedha zinazopatikana baada ya kusambaza dawa zifanye kazi ya kununulia dawa zingine kwa mahitaji mengine ya baadae.
Ameipongeza MSD kwa kazi kubwa inayofanya nchini na kuwataka kuendelea kuchapa kazi hiyo kwa weledi, ari na umakini mkubwa kwa sababu kazi ikifanyika vizuri na malengo ya afya bora kwa watanzania yatafikiwa vizuri nchini kote.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...