Na Mwashungi Tahir
Imeelezwa kwamba idadi walioingia nchini kwa mwezi wa January 2020 ni 58.761 sawa na ongezeko la asilimia 27.4 ikilinganishwa na wageni 46,133 walioingia mwezi wa January mwaka 2019.
Hayo amewasilisha Raya Mohammed Mahfoudh Afisa Takwimu Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali huko katika Ukumbi wa Ofisi ya Mtakwimu wa Serikali uliopo Mazizini wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uingiaji wa wageni Zanzibar.
Amesema Nchi inayoongoza kuleta wageni ni Italia ambapo jumla ya wageni 8,903 asilimia 15.2 waliwasili Zanzibar , ikifuatiwa na Ufaransa asilimia 7.8 na Marekani asilimia 5.7
Pia amesema kwa upande wa Bara la Ulaya asilimia 67.7 ya wageni walioingia mwezi wa January 2020 ambapo sawa na ongezeko la asilimia27.2 ikilinganishwa na mwezi wa January mwaka 2019.
Aidha amesema wageni 28,634 waliongia nchini ni wanaume na wageni 30,127 ni wanawake ambapo asilimia 5,2 ya wageni walikuwa na umri chini ya miaka 15, asilimia 86.2 ni wenye umri wa miaka 15-64 na asilimia 8.6 ni wenye umri kuanzia miaka 65+.
Kwa upande wake Kamisheni ya Utalii Afisa Masoko Maabadi Jaffar Muhidini amesema sababu zinazopelekea kuongezeka wageni Zanzibar ni pamoja na kuwepo vivutio vingi vya kutembelea wageni na kuwepo kwa amani na utulivu .
Pia alisema sababu nyengine ni kuwepo kwa hoteli kubwa kama vile Park Hayat , Serena na vile vile wataliana ndio wa mwanzo kutembelea Zanzibar hasa sehemu za Kaskazini Kiwengwa ambapo kuna hoteli nyingi za kisasa.
Nae Abdul-malik Bakari Ali Mkuu wa Kitengo cha Takwimu za Utalii Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali amesema taarifa hizo zinapatikana kila mwezi kutokana na ukusanyaji wa wageni nchini na kuhakikisha jamii wanazipata kwa uhakika jinsi ya uingiaji wa wageni hao.
Afisa Takwimu Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Raya Mohmed Mahfudhi
akitoa Takwimu za uingiaji wa wageni kwa mwezi Januari 2020 imeonesha
kupanda kwa wageni 58,761 sawa na ongezeko la asilimia 27.4
ikilinganishwa na wageni 46,133 walioingia mwezi Januari 2019, hafla
iliofanyika Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Mazizini Mjini Zanzibar.
Baadhi ya Waandishi wa Habari waliohudhuria katika Mkutano wa Takwimu za
uingiaji wa wageni (watalii) kwa kwaka 2020 wakifuatilia tarifa ya
takwimu hizo.
Muandishi wa habari kutoka Dailynews Issa Yusuf akiuliza maswali katika
Mkutano wa Takwimu za uingiaji wa wageni Nichini kwa mwaka 2020. Hafla
iliyofanyika Ofisi za Mtakwimu Mkuu wa Serekali Mazizini Mjni Zanzibar.
Mkuu wa Kitengo cha Takwimu za Utalii Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serekali Abdulmalik Bakari Ali akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wandishi wa habari. Picha na Makame Mshenga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...