Prisca Richard Masanja, mwanafunzi wa chuo cha Diplomasia cha Dar es Salaam, ameibuka mshindi wa taji la Miss Utalii mkoa wa Pwani mwaka 2020 ( Miss Tourism Coast Region 2020), katika kinyang'anyilo maalum kilicho fanyika katika hoteli ya kitalii ya Regency Park ,tarehe 26 ,Februari 2020, na kushirikisha jumla ya washiriki 13. 
 
Kwa ushindi huk Prisca Richard Masanja(6), pamoja na washindi wa 2- 5 ,watawakilisha mkia wa pwani katika fainali za kanda za Miss Utalii kanda ya Pwani ya Kaskazini 2020 ( Miss Tourism North Cost Circuit 2020), wakiungana na washindi wa 1- 5 wa mikoa ya Dar es Salaam na Tanga Katika kinyang'anyilo hixho cha Miss Utalii mkoa wa Pwani, ushindani ulikuwa mkali kutokana na washiriki karibu wote kukaribiana kivigezo na sifa. 
 
Elizabeth Samwel Munatta (8) aliibuka mshindi wa pili,huku Lucy Laurent Shirima (1) akiibuka mshindi wa tatu,Mariam Ahmed Kimaro (7) akishika nafasi ya nne,na Jesca Japhet Msechu(5) akiibuka mashindi wa tano. NB:Namba zilizo kwenye mabano ni namba aliyovaa kila mahiriki wakayi wa shindano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...