Naibu Waziri wa Afya wa Iran amethibitisha kuwa amepatwa na virusi vya Corona lakini amesisitiza kuwa, nchi hii itashinda janga la virusi hivyo wiki chache zijazo.

Iraj Harirchi amesema, kwa sasa amewekwa katika karantini ambako anapewa matibabu na kwamba hali yake ya kiafya ni nzuri kwa ujumla japokuwa anasumbuliwa na homa na uchovu.

Harirchi amesema ana uhakika kwamba, Iran itashinda mlipuko wa virusi vya Corona katika wiki kadhaa zijazo akisisitiza kuwa, nchi hii ina zana na matibabu madhubuti.

Kesi za virusi vya Corona nchini Iran zilianza kurekodiwa katika mji wa Qum ulioko katikati mwa nchi na hadi sasa vimesababisha vifo vya watu 15. Watu wengine 95 wameambukizwa virusi hivyo.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...