ILI Kufikia uchumi wa kati katika sekta ya Viwanda, mahitaji ya wakulima, wavuvi na wafugaji hayawezi kutekelezwa kwa bajeti ya serikali pekee bali wadau wakubwa wajitokeze kuwekeza.

Hayo yamesemwa wakati wa Mkutano wa wadau katika Kuongeza tija kwenye sekta ya kilimo na mifugo kwa maendeleo ya Viwanda.

Mkutano huo uliodhaminiwa na  Benki ya Biashara ya NBC, umeweza kuhudhuriwa na Waziri wa Viwanda na Biashara  Innocent Bashungwa, Waziri wa Ufugaji na Uvuvi Luhaga Mpina na Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe.

Benki ya NBC imesema kuwa itaendelea kushirikiana na kuwasaidia wakulima hasa katika kuwapatia mbinu mbalimbali za kuboresha ,  mazao  na mbegu zao kwa lengo la kuhimarisha sekta hiyo.

Mkuu wa Kitendo cha Wafanyabiashara wadogo na wa kati benki ya NBC, Evance Luhimbo amesema benki hiyo imekuwa mbele kuwasaidia wakulima wadogo, wa kati na wakubwa.

Amesema mikakati yao ya mbeleni kwenye kilimo ni kuhakikisha wanaisaidia sekta hiyo kwa asilimia kubwa na kwa kuanzia wameaandaa nyaraka inayoelezea ni kwa jinsi gani mtu anaweza kumsaidia mkulima katika mazao yake na mtaji wake.

"Tunaowataalamu wengi ambao  tunaendelea kuwatumia  kuwasaidia wakulima lakini NBC tunashirikiana na PASS ambao kazi yao kubwa kuwawekea ulinzi na usalama wa mazao wakulima," amesema 

Aidha, Bashe amesema kuwa katika sekta ya Kilimo kumekuwa na changamoto kubwa ya bajeti, kwani haiwezi kutosheleza kwenye kuleta maendeleo ya kilimo na kufikia malengo yaliyowekwa na serikali.

Amesema, amewataka mabenki wasitoe mikopo mikubwa sana kwa wakulima kwani wamekuwa wanawakopesha sawa na wafanyabiashara wengine jambo linalopelekea wakulima hao kushindwa kulipa kwa wakati.

Waziri wa Viwanda Bashungwa, amesema katika mwaka 2014-2019 wameingiza chakula tani Trilion 1.3 jambo ambalo serikali kwa sasa linaangalia namna ya kuhakikisha uingizaji wa chakula toka nje kinapungua.

Pia, serikali imeweka mkakati katika kukuza sekta ya viwanda kutoka asilimia 25 hadi 35 katika uzalishaji na kupunguza uingizwaji wa chakula kutoka nje ya nchi.

Naye Waziri Mpina ameeleza kuwa kuna fursa kubwa sana katika sekta ya mifugo na uvuvi ila haijaelekezwa, mvuvi anapata hasara kutokana na kukosa mahali pa kuanika au kukausha  na huu ndiyo wakati wa wajasiriamali kuwekeza.
 Waziri wa Ufugaji na Uvuvi akikata utepe kuashiria kuzindua kitabu chenye muongozo wa sekta ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi wakati wa Mkutano wa wadau katika Kuongeza tija kwenye sekta ya kilimo na mifugo kwa maendeleo ya Viwanda wa siku mbili Feb 27-28 unaofanyika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere JNICC na kudhaminiwa na Benki ya Biashara ya Taifa NBC.
 Waziri wa Viwanda na Biashara  Innocent Bashungwa (wa tatu kushoto) Waziri wa Ufugaji na Uvuvi Luhaga Mpina ( wa tatu kulia)  na Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe (katikati) sambamba na Viongozi wa Bodi ya maendeleo ya Kilimo wakionesha kitabu kilichozinduliwa chenye muongozo wa kuleta tija ya maendekeo katika sekta ya kilimo na mifugo kwa maendeleo ya Viwanda. Mkutano huo wa siku mbili Feb 27-28 unafanyika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere JNICC na kudhaminiwa na Benki ya Biashara ya Taifa NBC.

 Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe akichangia mada wakati wa Mkutano wa wadau katika Kuongeza tija kwenye sekta ya kilimo na mifugo kwa maendeleo ya Viwanda wa siku mbili Feb 27-28 unaofanyika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere JNICC na kudhaminiwa na Benki ya Biashara ya Taifa NBC.
 Mkuu wa Kitendo cha Wafanyabiashara wadogo na wa kati benki ya NBC, Evance Luhimbo akizungumza na waandishi wa habari na kuelezea mikakati ya benki hiyo katika kuendelea kuwasaidia wakulima katika uzalishaji bora, Hayo ameyasema wakati wa Mkutano wa wadau katika Kuongeza tija kwenye sekta ya kilimo na mifugo kwa maendeleo ya Viwanda wa siku mbili Feb 27-28 unaofanyika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere JNICC na kudhaminiwa na Benki ya Biashara ya Taifa NBC.
 Waziri wa Ufugaji na Uvuvi Luhaga Mpina akichangia mada wakati wa Mkutano wa wadau katika Kuongeza tija kwenye sekta ya kilimo na mifugo kwa maendeleo ya Viwanda wa siku mbili Feb 27-28 unaofanyika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere JNICC na kudhaminiwa na Benki ya Biashara ya Taifa NBC.
 Wadau mbalimbali wa maendeleo wakiendelea kusikiliza Mkutano wa wadau katika Kuongeza tija kwenye sekta ya kilimo na mifugo kwa maendeleo ya Viwanda wa siku mbili Feb 27-28 unaofanyika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere JNICC na kudhaminiwa na Benki ya Biashara ya Taifa NBC.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...