Mkuu wa Kituo cha Mawasiliano ya Umma na Upashaji Habari cha Wizara ya Afya nchini Iran, amethibitisha habari ya kufariki dunia watu wawili kutokana na maambukizi ya virusi vya Corona mjini Qom nchini hapa.

Kiyanush Jahanpur aliyasema hayo jana Jumatano na kubainisha kwamba kufuatia ongezeko la matatizo ya kupumua lililoshuhudiwa katika siku za hivi karibuuni mjini Qom, uchunguzi wa vipimo ulithibitisha kesi mbili za maambukizi ya virusi vya Corona.
 
 Ameongeza kwa kusema: "Kwa bahati mbaya watu wawili ambao ni wazee na kutokana na upungufu wa vifaa vya tiba katika wodi maalumu za hospitali za mji huo, walipoteza maisha yao kwa maradhi hayo." 
 
Wakati huo huo Ali Larijani, Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) jioni ya jana alizungumza kwa njia ya simu na Waziri wa Afya, Tiba na Mafunzo ya Udaktari wa Iran, Saeed Namaki ambapo sambamba na kumueleza kuwa amepata taarifa za kuthibitika kesi mbili za ugonjwa unaotokana na virusi vya Corona mjini Qom, alitaka kuchukuliwa hatua za dharura kwa ajili ya kuzui na kuwatibu waathirika wa maradhi hayo.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...