Kamanda wa polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Iringa  SP. Yusuf Kamote (pichani kulia) akiongea na madereva wa vyombo vya moto kwenye kampeni ya usitumie kilevi na kuendesha chombo cha moto iliyoratibiwa na kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Limited SBL mjini Iringa leo.
Kamanda wa polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Iringa  SP. Yusuf Kamote (pichani kulia) akimvisha Kiakisi mwanga Mwenyekiti wa Umoja wa Bodaboda Iringa, Juma Gamba wakati wa uzinduzi wa kampeni ya usitumie kilevi na kuendesha chombo cha moto iliyoratibiwa na kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Limited, hafla iliyofanyika katika viwanja vya Stendi ya Daladala Manispaa ya Iringa leo. Pichani kushoto ni Meneja mahusiano wa SBL, Neema Temba.


Iringa, Februari 1, 2020 –
Maelfu ya wakazi wa mji wa Iringa na maeneo ya jirani, ikiwa ni pamoja na watumiaji barabara, madereva wa magari binafsi na ya usafiri wa umma wamepatiwa elimu ya usalama barabarani kupitia kampeni inayoendeshwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) kwa kushirikia na Jeshi la Polisi, Kitengo cha Usalama Barabarani.

Ikijulikana kama ‘Usitumie Kilevi na Kuendesha Chombo cha Moto’, kampeni hii inalenga kuiunga mkono Serikali katika kuhamasisha usalama barabarani ili kuepusha ajali zinazosababishwa na matumizi ya vilezi na kuendesha vyombo vya moto, alisema Mkurugenzi wa Mahusiano kwa Umma wa SBL , John Wanyancha.

“Kampeni hii inawalenga madereva wa mabasi ya abiria, waendesha bodaboda, waenda kwa miguu, wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu pamoja na wateja katika mabaa,” alisema Wanyancha.

Aliongeza “Usitumie Kilevi na Kuendesha Chombo cha Moto’ ni kampeni ya kitaifa inayolenga kuwaelimisha watumiaji wote wa barabara na haswa madereva juu ya unywaji wa kistarabu.

Katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, kampeni hii imeweza kufika katika mikoa kama Mwanza, Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Tanga Moshi na Arusha huku elimu iliyotolewa ikiwafikia takribani watu 100,000,”

Baadhi ya mbinu zinazotumika kufikisha ujumbe kwa umma juu ya usalama barabarani ni pamoja na redio, vipeperushi, makoti ya usalama barabarani, mabango, kuwafikia watu mmoja mmoja pamoja na kuwafikia watu kupitia vyombo vya habari kama televisheni na magazeti.

Akizungumza katika tukio la uzinduzi wa kampeni hiyo lililofanyika mjini Iringa, Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani Iringa Yusuph Kamota aliishukuru SBL kwa kuipeleka kampeni hiyo Iringa na kuongeza kuwa itasaidia kuongeza uelewa wa madereva na watumiaji wa barabara juu ya masuala ya usalama barabarani.

“Wote kwa pamoja kuanzia Jeshi la Polisi, madereva, jamii na wadau wengine tunajukumu la kuzifanya barabara zetu ziwe salama. Nimefurahi kuona kuwa pamoja na kwamba biashara yao ni ya kuuza pombe, wanalo jukumu la kuhamasisha unywaji wa kistarabu,” alisema RTO Kamota.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...