Waziri Mkuu wa Sudan ametangaza kuwa ameunda tume ya kuchunguza vitendo vya ukandamizaji vilivyofanywa na vikosi vya usalama vya nchi hiyo Alkhamisi na Ijumaa ya jana.

Akizungumza kwa njia ya televisheni, Abdalla Hamdok amesema kuwa: Nimechukua uamuzi wa kuunda kamati ya uchunguzi kufuatia matukio ya siku mbili zilizopita.

Waziri Mkuu Hamdok amesema kuwa, Mwanasheria Mkuu Taj-Elsir Ali ataongoza kamati hiyo ya uchunguzi ambayo inapaswa kutoa ripoti yake katika kipindi cha siku saba zijazo.

Maeneo yaliyoshuhudiwa maandamano makubwa zaidi Alkhamisi na Ijumaa ya jana ni mji mkuu Khartoum. Vikosi vya usalama siku ya Alkhamisi vilivamia maandamano ya wananchi hao na kuwatawanya kwa kutumia mabomu ya gesi ya kutoa machozi ambapo kwa akali watu 17 walijeruhiwa.

Raia hao walikuwa wakiandamana dhidi ya Baraza la Utawala linaloongozwa na Luteni Jenerali Abdul-Fattah al-Burhan.
 

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...