Zaidi ya shilingi Milioni 154 zimetumika kujenga vyumba vitatu vya madarasa na kukarabati shule ya Msingi Luagala 'B' Wilayani Tandahimba

Akizindua madarasa hayo Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Sebastian Waryuba amesema madarasa hayo yamewekwa na madawati tayari kwa wanafunzi kuendelea na masomo

"Tumezindua madarasa haya lakini pia wametukabidhi shule ikiwa katika muonekano unaovutia  ambapo kazi hii imefanywa na taasisi ya Eclat na Upendo ,"amesema Waryuba

Naye Mwenyekiti wa taasisi ya Eclat Toima Kiroya ameeleza kuwa katika mradi huo wameweza kujenga vyumba vitatu vya madarasa,kukarabati majengo 8,kisima chenye ujazo wa Lita 150,000,matundu 16 ya Choo,madawati 65,meza za walimu 16 na viti 16

Hata hivyo Dk Fred Heimbach wa Upendo Society kutoka Ujerumani ameeleza kuwa madhumuni ya ushirika huo ni kuboresha miundo mbinu katika sekta ya elimu

Sambamba na Hilo  Meneja wa mradi huo Msham Bashir ameishukuru serikali kwa kushirikiana  kuanzia ngazi ya Kijiji hadi Wilaya hivyo wananchi wanajukumu lankutunza miundo mbinu hiyo.
 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Sebastian Waryuba akizindua madarasa hayo akiwa na wafadhili waliowezesha mradi huo
 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Sebastian Waryuba na Mwenyekiti wa Eclat wakisaini makabidhino hayo
 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Sebastian Waryuba akikabidhi hati ya makabidhino Afisa Elimu Msingi Wilaya Hadija Mwinuka
 Matundu ya Choo kwa ajili ya wanafunzi na walimu Wao
Meneja wa mradi Msham Bashir (mzawa qa Luagala)ambaye ndiye aliwashawishi kuja kuboresha miundombinu ya Elimu Wilayani hapo
 Shule ya msingi Luagala 'B' katika muonekano mpya
 Wananchi wa Kijiji Cha Luagala 'B'wakishuhudia uzinduzi wa shule

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...