Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza hali ya dharura na kuufunga mji mkuu wa Kinshasa kujitenga katika hatua ya kupambana naa maambukizi ya virusi vya Corona.

Rais FĂ©lix Tshisekedi alitangaza kuchukua hatua hizo jana jioni kupitia televisheni ya taifa.

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo amesema kuwa, pamoja na kufunga mipaka ya nchi, kusitisha safari za ndani na nje ya mji mkuu zikiwemo za mabasi, ndege na majini, utekelezaji wa haraka unahitajika.

Mpaka sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeripotiwa kuwa na wagonjwa 48 wa covid-19 na watu watatu kufariki dunia kutokana na maambukizi ya ugonjwa huo.

Mji mkubwa wa pili wa taifa hilo, Lubumbashi, ulifungwa kwa saa 48-siku ya Jumatatu baada ya watu wawili kutambuliwa kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona.

Mmoja alikuwa mwanamume mwenye miaka 47 na mtoto wake wa kiume wa miaka 13, walikuwa wametokea mji mkuu wa Kinshasa siku ya Jumapili.
 
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...