Katibu Mkuu wa Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, akitoa
maelekezo kwa Uongozi wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) wakati
alipotembelea mradi wa ujenzi wa meli mpya, chelezo na Ukarabati wa Meli
ya MV Victoria jijini Mwanza, Mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mkurugenzi
Mkuu wa Kampuni hiyo, Eric Hamissi.
Katibu Mkuu wa Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, akitoa
maelekezo kwa Uongozi wa Kampuni ya KTMI ya Korea Kusini inayofanya
ukarabati wa meli Meli ya MV Victoria jijini Mwanza, Mwishoni mwa wiki,
wakati alipotembelea maendeleo ya ujenzi wake.
Muonekano wa Chelezo inayojengwa katika bandari ya Mwanza South ambayo
ujenzi wake umefikia asilimia 96. Kukamilika kwa chelezo kutarahisisha
matengenezo ya meli katika Ziwa Victoria.
Katibu Mkuu wa Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, akimsikiliza
Muwakilishi wa Kampuni ya KTMI ya Korea Kusini, inayojenga meli mpya
katika bandari ya Mwanza South wakati akimweleza hatua iliyofikiwa ya
ujenzi wa meli, wakati Katibu Mkuu huyo alipotembelea maendeleo ya
ujenzi wake mwishoni mwa wiki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...