Katibu Mkuu wa Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, akitoa maelekezo kwa Uongozi wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa meli mpya, chelezo na Ukarabati wa Meli ya MV Victoria jijini Mwanza, Mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Eric Hamissi.
 Katibu Mkuu wa Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, akitoa maelekezo kwa Uongozi wa Kampuni ya KTMI ya Korea Kusini inayofanya ukarabati wa meli Meli ya MV Victoria jijini Mwanza, Mwishoni mwa wiki, wakati alipotembelea maendeleo ya ujenzi wake.
 Muonekano wa Chelezo inayojengwa katika bandari ya Mwanza South ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 96. Kukamilika kwa chelezo kutarahisisha matengenezo ya meli katika Ziwa Victoria.
 Katibu Mkuu wa Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, akimsikiliza Muwakilishi wa Kampuni ya KTMI ya Korea Kusini, inayojenga meli mpya katika bandari ya Mwanza South wakati akimweleza hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa meli, wakati Katibu Mkuu huyo alipotembelea maendeleo ya ujenzi wake mwishoni mwa wiki.

Muonekano wa meli ya MV Victoria mara baada ya ukabati mkubwa ambao mpaka sasa umefikia asilimia zaidi ya 96. Meli hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 1,200 na mzigo wa tani 200.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...