KIKAO cha Kamati ya Uongozi cha TFF kimeazimia kuwa, baada ya siku 30 serikali itakaporuhusu michezo kuendelea, mechi za ligi kuu, ligi daraja la kwanza, ligi daraja la pili na ligi ya mabingwa wa mikoa (RCL) zitachezwa bila watazamaji, ili kudhibiti kusambaa kwa virusi vya Corona.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Almas Kasongo mara baada ya kikao hicho ambacho kimehudhuriwa pia na Rais wa TFF, Wallace Karia.

Kasongo amesema pia kuwa wachezaji wote watafanyiwa vipimo maalum kuchunguzwa endapo wameathirika na virusi vya Corona au la kabla ya ligi hizo kurejea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...