Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa (Mb) leo tarehe 30 Machi, 2020 amepokea kifaa maalumu cha kunawia mikono kilichotengenezwa na mjasiriamali wa kitanzania ndugu. Jonas Urio (Ambaye anatokea katika mkoa wa Manyara).
 
Akizungumza leo Waziri Bashungwa amempongeza Jonas Urio kwa ubunifu wake huo wa kutengeza kifaa kizuri na bora cha kunawia mikono ambacho kinaweza kutumiwa na taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kuhudumia watu mbalimbali kusafisha mikono yao ili kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona.

Kwa upande wake Mjasiriamali Jonas Urio ambaye ni mbunifu wa teknolojia hii ameishukuru Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kumpa ushirikiano tangu awali alipoanza ubunifu wake hadi kufikia hatua hii ambapo ameshasajiliwa na ubunifu wake utambulika.
 
Jonas amesema, “Napokea ushauri wa maboresho ya kifaa hiki niliyopewa na Waziri na Naibu waziri ambao wote kwa pamoja wamefurahia sana ubunifu wangu, naahidi kufanyia kazi maboresho yote haraka ili kifaa hiki kingie sokoni ili kusaidia wananchi kujisafisha mikono na kupambana na ugonjwa huu wa Corona”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...