Katibu Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) amesema kuwa idadi ya watu walioathiriwa na virusi vya corona barani Afrika imepita watu 2,600.

Tedros Adhanom Ghebreyesus ameviambia vyombo vya habari kwamba, idadi ya watu walioambukizwa virusi vya corona barani Afrika imefikia 2,650 na kwamba wagonjwa wasiopungua 49 miongoni mwao wameaga dunia.

Katibu Mkuu wa Shirika la Afya Duniani amesema kuwa, shirika hilo liko tayari kuzisaidia nchi zote za Afrika na kuongeza kuwa: Nchi zenye mifumo dhaifu ya afya zinalazimika kuchukua hatua madhubuti za kudhubiti maambukizi ya virusi vya corona wakati zinapogundua kesi ya kwanza ya maambukizi ili kuzuia kusambaa zaidi virusi hivyo. 
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...