Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Dar
es Salaam na Pwani DAWASA wamechukua tahadhari kwa wafanyakazi dhidi ya
Maambukizi ya homa ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona.
Dawasa
wamechukua tahadhari hiyo kwa kuwapatia wafanyakazi wake wakiwemo
mafundi wa maeneo mbalimbali vifaa vya kuwakinga ikiwemo Barakoa ili
wavae muda wote wakiwa katika majukumu yao.
Hatua
hiyo ni muhimu katika kutii agizo la serikali kwa kuvaa barakoa ili
kuweza kujikinga, kupunguza maambukizi pamoja na kuwalinda wengine pindi
wanapotoa huduma kwa jamii.
Afisa biashara msaidizi DAWASA Noel Kipera akisoma
mita ya mteja katika eneo la Kimara stop over huku akiwa amevaa
(barakoa), kifaa cha kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.
Dawasa inahakikisha usalama wa watumishi wake dhidi ya maambukizi ya
Corona.
Mafundi wa DAWASA Mkoa wa Ubungo wakizibiti uvujaji
katika eneo la Mbuzi 40 Kimara kwa kubadilisha mabomba ya nusu inchi.
Mafundi hao wametii agizo la serikali kwa kuvaa barakoa kujikinga na
maambukizi dhidi ya virusi vya Corona.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...