NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA
MKUU
wa wilaya ya Kibaha,mkoani Pwani Assumpter Mshama ,amewaasa wazazi na
walezi kuwakalantin watoto wao kwa kuwasimamia wabaki majumbani,pamoja
na kujiendeleza kujisomea pasipo kudhurura magulioni wala mitaani .
Amesema
serikali imeshachukua hatua ili kujilinda na corona ,hivyo kuwaacha
watoto hao wadhurure badala ya kutulia kujilinda nyumbani itakuwa ni
hatari kwa afya zao.
Akiendelea
kukumbushia umuhimu wa kijilinda dhidi ya ugonjwa wa corona kwa
jamii,Assumpter alisema, pia ngoma na midundiko haina nafasi kwa sasa
kujiepusha na mikusanyiko.
Pamoja
na hilo,kamati ya maendeleo ya Kata ya Visiga wilayani Kibaha, nayo
imetoa elimu ya kujikinga na ugonjwa huo kwa wafanyakazi kwenye
viwanda.
Mtendaji wa
kata hiyo ,Aloisia Nyelo alisema kuwa wamefikia hatua hiyo baada ya
kuona kuwa baadhi ya wafanyakazi wa viwandani hawana elimu ya kutosha
juu ya maambukizi ya ugonjwa huo.
Alisema
kuwa ,pia wametembelea mitaa yote iliyopo kwenye kata hiyo kwa kupitia
nyumba kwa nyumba na mkutano na hadi sasa wameshatoa elimu kwa wananchi
zaidi ya 15,000 .
Nae
Mwenyekiti wa mtaa wa Zegereni Rashid Likunja alisema , janga hilo la
Corona ni kama vita hivyo lazima wananchi wote wapate taarifa ndiyo
maana wameamua kupita maeneo mablimbali ikiwemo viwandani.
Awali
Diwani wa kata Kambi Legeza alisema kuwa mbali ya kutoa elimu hiyo pia
walikagua changamoto ya ubovu wa barabara ya kwenda viwandani kwani ni
kero kubwa .
Kamati hiyo
ilitembelea viwanda kikiwemo cha cha Gypsum cha BNBM, Hong You Steel Co
Ltd na maeneo mbalimbali ya mtaa wa Zegereni.
MKUU
wa wilaya ya Kibaha,mkoani Pwani Assumpter Mshama
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...