Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

NAIBU Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndugulile amewashauri watu wenye magonjwa sugu kuchukua tahadhari zaidi hasa kwa kupima afya na kufuata ushauri wa wataalamu katika kukabiliana na ugonjwa unaosababishwa na virusi vya  Corona (Covid -19.) ambao hadi sasa maambukizi yake nchini yamefika watu 32 na vifo vitatu.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Ndugulile amechapisha taarifa iliyoeleza kuwa mtu mwenye magonjwa sugu ikiwemo kisukari, shinikizo la damu, pumu, ugonjwa wa moyo na unene uliopitiliza huathirika zaidi na Covid-19.

Aidha Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa mtu mwenye magonjwa hayo yupo kwenye hatari zaidi na wanaweza kupoteza maisha na
amewashauri watu kuchukua tahadhari zaidi kwa kupima afya na kuzingatia ushauri wa kitaalamu juu ya magonjwa hayo ili kupunguza madhara zaidi katika kipindi hiki ambacho dunia inapambana katika kukabiliana na janga hilo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya, leo Aprili 10, 2020 jumla ya watu walioambukizwa ugonjwa wa corona imefika 32, na waliofariki dunia kutokana na ugonjwa huo imefikia watatu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...