Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

MAUAJI ya Kimbari ya mwaka 1994 ambayo yanaelezwa kuwa ni mpango uliotekelezwa na baadhi ya watu na kuuwa maelfu ya watu wa kabila la Watutsi nchini Rwanda, mmoja ya watekelezaji wa tukio hilo  Felician Kabuga aliyekamatwa baada ya miaka 26 tangu kutokea kwa tukio hilo ameieleza mahakama inayomshikilia  nchini Ufaransa kuwa wampe dhamana wakati akisubiri ni wapi kesi yake itasikilizwa aidha Ufaransa alipokamatwa au nyumbani anakodaiwa kutekeleza mauaji hayo.

Felician aliyekwepa mkono wa dola kwa miaka 26 anatuhumiwa kwa makosa 11 ikiwemo kufadhili mpango wa utekelezaji wa mauaji ya Kimbari mpango uliogharimu maisha ya watu zaidi ya milioni moja wa kabila la watutsi kwa siku 100, Kabuga alifika mahakamani hapo akiwa katika kiti cha magurudumu na kuiomba mahakama hiyo imuachie  huru kwa kuwa afya yake  si nzuri na ni mzee ana miaka 87 huku nyaraka zote zikionesha ana umri wa miaka 84.

Aidha Kabuga ameieleza mahakama hiyo kuwa hakuhusika na mauaji ya mtusi yetote bali alikuwa anafanya nao kazi.

Kabuga anadaiwa kufadhili silaha kwa watu wa jamii ya wahutu ambao walitekeleza mauaji hayo ya mwaka 1994 na kutokomea kusikojulikana hadi alipokuja kukamatwa mwaka huu nchini Ufaransa ambapo pia Marekani iliweka dau la dola milioni tano kwa yeyote atakayetoa taarifa za wapi alipo Kabuga.

Felician Kabuga alikuwa mfanyabiashara maarufu akizalisha zao la chai nchini Rwanda na alimiliki makampuni mengi yaliyotoa ajira nchini humo na nje ya nchi, pia alimiliki  kituo binafsi cha redio ambacho kinashutuhumiwa kurusha habari zilizokuwa zikihamasisha wahutu kuwauwa watutsi.

Kabuga ambaye alikuwa rafiki wa karibu wa kiongozi wa chama tawala Rais nchini humo Juvenal Habyarimana ambaye ni mkwe wake aliyefariki mwaka 1994 anadaiwa kutumia utajiri na biashara kupanga na kufadhili mauaji hayo. 

Kesi hiyo imehairishwa hadi Juni tatu baada ya mahakama kutupilia mbali maombi ya dhamana yaliyotolewa na Kabuga yakihusisha afya na uzee.

Felician Kabuga amekana madai hayo ikiwa alikimbia nchini mwake na kujificha huku akitumia majina ya uongo ili tu asikamatwe kwa miaka 26, je ataachiwa huru? na ikiamuliwa kesi ikasomwe nchini mwake hisia za raia wa Rwanda hasa watutsi itakuaje?

Kwa ufupi Felician  Kabuga alizaliwa Julai 9, 1935 huko Mukarange nchini Rwanda, huku akiwa tajiri mkubwa na mfanyabiashara ambapo kabla ya kutajwa kuhusika na tukio hilo mwaka 1995 alianzisha Kampuni ya biashara nchini Kenya jambo ambalo aliyekuwa Rais wa Marekani Barack Obama alipotembelea Kenya mwaka 2008 hakulibariki, kwa kuwa hata mpelelezi nchini humo aliyejitokeza kusaidia  kupatikana kwa Kabuga aliishia kuuawa. 

Mwaka 2020 jumamosi ya tarehe I6 Kabuga alikamatwa katika moja ya viunga huko Paris Ufaransa na kuwekwa kwa muda katika gereza la La Sante'.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...