NA MWAMVUA MWINYI,PWANI
MKOA
wa Pwani, umekemea wakulima wa ufuta waliofanya udanganyifu msimu wa
ununuzi uliopita kwa kuchanganya ufuta na mchanga, kwani umesababisha
doa kwenye soko hivyo kwasasa mfumo utakaotumika ni wa stakabadhi
ghalani ,ambao utadhibiti udanganyifu na kuinua pato la mkulima.
Aidha
minada ya ununuzi wa ufuta mwaka huu yatafanyika kupitia mfumo huo na
kwa njia ya kielektroniki kupitia soko la bidhaa Tanzania (TMX).
Akifungua
kikao cha kujadili maandalizi ya msimu wa ununuzi wa ufuta kupitia
mfumo wa stakabadhi ghalani ,mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist
Ndikilo aliwataka wakulima kuacha udanganyifu ili kurudisha imani kwa
wanunuzi na mkulima mwenyewe kuondokana na maumivu ya bei
zilizokandamizi .
"Mkoa
unatambua changamoto zilizojitokeza msimu wa ununuzi wa mwaka 2019/2020
,ikiwemo udanganyifu ,baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika vya
msingi (AMCOS kutokuwa waaminifu pamoja na ubora duni wa miundombinu ya
maghala na ucheleweshaji wa zoezi la usafirishaji ufuta kutoka kwenye
maghala "; alifafanua Ndikilo .
Ndikilo alieleza ,changamoto hizo zilisababisha wadau kulalamikia ufanisi mdogo wa mfumo mzima wa ununuzi wa zao hilo .
Mkuu
huyo wa mkoa alisema ,ili kukabiliana na changamoto hizi serikali
imeamua kuanzisha mfumo wa stakabadhi ghalani kuanzia msimu huu .
Ndikilo
alibainisha kupitia mfumo ,wanachama na wakulima watapeleka ufuta
kwenye maghala ya vyama vya ushirika vya msingi ambavyo vitapeleka ufuta
kwenye maghala makuu yaliyosajiliwa na bodi ya leseni za maghala
Tanzania ,huku maghala makuu yatapeleka taarifa za ufuta uliopokelewa
kwenda TMX ambayo itaratibu minada .
Ndikilo
alielekeza pia ,wakulima walipwe katika akaunti zao na wakala wa vipimo
wasimamie ubora wa mizani ili wakulima wasipunjwe .
Hata
hivyo ,aliwaelekeza viongozi na watendaji wa vyama vya ushirika
wahakikishe vifungashio vya ufuta ghafi vinapatikana kwa wakati kwa
wakulima.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...