Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe
Magufuli akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika katika Ukumbi wa
Baraza la Mawaziri Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma. Kikao hicho kimehudhuriwa pia
na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa,
Mawaziri pamoja na Manaibu Mawaziri leo tarehe 27 Mei 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe
Magufuli akiwa amesimama kwa dakika moja pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia
Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mawaziri pamoja na Manaibu
Mawaziri ili kumkumbuka na kumuombea aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Marehemu
Balozi Augustine Mahiga kabla ya kuanza kwa Kikao cha Baraza la Mawaziri Ikulu
ya Chamwino mkoani Dodoma. PICHA NA IKULU
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...