Tume ya uchaguzi nchini Burundi imemtangaza mgombea wa chama tawala Meja Jenerali Evariste Ndayishimiye kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika juma lililopita.

Meja Jenerali Ndayishimiye ameshinda kwa kupata 68.72% ya kura zilizopigwa, wakati Agathon Rwasa, kutoka chama kikuu cha upinzani akipata 24.19% , kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na tume hiyo.

Kwa kuwa Meja Jenerali Ndayishimiye amepata zaidi ya 50% ya kura, ameepuka kufanyika kwa duru ya pili ya uchaguzi.

Haya ni matokeo ya awali ya uchaguzi , ambapo matokeo ya mwisho yatatangazwa na mahakama ya kikatiba tarehe 4 mwezi Juni.

Meja Jenerali Ndayishimiye aliteuliwa kupeperusha bendera ya chama cha CNDD-FDD katika kikao kisicho cha kawaida kilichofanyika Gitega, mji mkuu wa kisiasa baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa saa tatu ya chama tawala cha CNDD-FDD.

Wagombea wengine waliochuana 

kwenye kinyang'anyiro hicho ni pamoja na;

Gaston Sindimwo (Uprona) - 1.64%

Domitien Ndayizeye (Kira Burundi) - 0.57%

LĂ©once Ngendakumana (FRODEBU) - 0.47%

Nahimana Dieudonné - 0.42%

Francis Rohero - 0.20%
HABARI KWA HISANI YA BBCSwahili.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...