Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Sharmillah
Sarwatt amewataka wadau mbalimbali wanaohusika mashauri na haki za watoto
kushirikiana ili kuweza kutatua changamoto
zilizopo katika mahabusu na baadhi ya magereza ili hakikisha mtoto
anapatiwa haki kwa wakati na katika mazingira bora, ikiwemo kulindwa.
Akizungumza leo wakati akifungua kikao kazi cha
wadau wa Mahakama baada ya kufanyika ukaguzi wa mahabusu za watoto na baadhi ya
magereza ulifanyika kuanzia Machi 16 hadi Machi 25, mwaka huu kilichofanyika
kwenye Kituo cha Habari cha Mahakama ya Tanzania (JMC, kilichopo Mahakama Kuu
ya Tanzania, Dar es Salaam.
Alisema moja ya jukumu la Mahakama Kuu Masjala Kuu
ni kukagua Mahakama zote za chini,magereza na mahabusu za watoto nchini ili
kuboresha huduma za Mahakama kwa kuhakikisha haki inapatikana kwa wote na kwa
wakati
Msajili huyo alisema kila mdau ana wajibu wa
kufanikisha haki ya mtoto inapatikana kwa wakati, ikiwemo kutafuta suluhisho la
changamoto zilizojitokeza katika ukaguzi huo kwa haraka.
“Miongoni
changamoto iliyojitokeza katika ukaguzi huo kuna baadhi ya watoto walikutwa
katika gereza la watu wazima kwa sababu ya kushindwa kutathimini umri wao
wakati wa kuaandaa hati zao za mashtaka na hivyo kusomeka ni watu wazima. Katika
suala hili ni jukumu la kila mdau kuweza kuangalia jinsi ya kulitatua,” alisema
Mhe. Sarwatt.
Kwa Naibu Msajili wa Mahakama wa Kuu ya Tanzania
Dawati la Watoto, Mhe. Nyigulila Mwaseba alizitaja changamoto nyingine zilizopo
katika ukaguzi huo, kuwa ni watoto
waliokinzana na sheria kupigwa wakati wa
kukamatwa hali inayowasababishia baadhi yao kupata ulemavu wa kuhudumu hasa
katika mkoa wa Dare es Salaam,
kutokuwepo kwa mahabusu za watoto hali inyosababisha watoto kuchanganywa
na watu wazima katika magereza.
Nyingine Maafisa Ustawi wa Jamii hawahusishwi katika
hatua za ukamataji wa watoto ili haki zao za msingi zifuatwe, baadhi ya majengo
ya mahabusu ni chakavu na yana maeneo finyu hivyo kuwanyima uhuru watoto na
nafasi ya kujifunza kwa vitendo,ikiwemo kuwabadilisha tabia, upungufu wa
Maafisa Ustawi wa Jamii, kutokuwepo kwa fungu la kuwahudumia watoto waliokutana
na sheria magerezani( watoto waliopo gerezani baada ya mama zao kutumiwa na
kosa la jinai au kufungwa) na kutokuwepo kwa usafiri katika mahabusu za watoto
na kusababisha kutofikishwa mahakamani kwa wakati.
Akichangia hoja kuhusu kuwepo kwa bajeti au fungu la
kuwahudumia watoto waliokutana na sheria magerezani (waliopo gerezani baada ya
mamazao kutuhumiwa na kosa la jinai au kufungwa na kuwarekebisha watoto
waliokinzana na sheria, ikiwemo kuwepo kwa mazingira wezeshi ya kusomea. Mrakibu
Mwandamizi wa Magereza, Amina Kavirondo alisema kuna haja ya kupaza sauti ili
bajeti kwa ajili hiyo itengwe kwa ajili hiyo.
Wadau hao, pia walipendekeza kuwepo kwa mikakati ya
kuanzisha mahabusu za watoto waliokinzana na sheria.
Ukaguzi huo ulifanyika baada ya Jaji Kiongozi kuteua
timu ya watu sita, ambayo ilifanya kazi hiyo kwenye mahabusu nne za watoto.zilizopo
mikoa ya Dar es Salaaam, Tanga, Moshi, Arusha na Mbeya, Shule ya Maadilisho
iliyopo Irambo – Mbeya na baadhi ya magereza ambayo ni gereza la Maweni,
Karanga, Ruanda, Kisongo, Chumbageni.
Jumla vituo 13 na watoto 131 walihusika katika
ukaguzi huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...