Na Zainab Nyamka
TIMU ya Namungo ya Lindi imekuwa timu ya kwanza kutinga hatua ya nusu fainali ya Kombe la Azam Sporta Federation CuP ASFC.
Katika mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Majaliwa Ruangwa, Namungo wamefanikiwa kuibuka na ushindu wa goli 2-0 dhidi ya Alliance
Baada ya matokeo hayo, Namungo wanasubiri mshindi kati ya Sahare All Stars dhidi ya Ndanda utakaochezwa kesho Mkoani Tanga.
Mchezo wa pili wa ASFC unapigwa majira ya saa 1 usiku kati ya Yanga na Kagera katika Uwanja wa Taifa ambapo mshindi wa mchezo huo atamsubiri Mshindi kati ya Simba na Azam.
Simba atacheza kesho dhidi ya Azam katika Uwanja wa Taifa majira ya saa 1 usiku.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...