Tume ya Utumishi wa Umma inapenda
kuwajulisha watumishi wa umma na wananchi wote kuwa kuanzia leo tarehe 16 hadi
23 Juni 2020, itakuwa inapokea na kusikiliza
kero na malalamiko ya watumishi wa umma kuhusu masuala mbalimbali ya
kiutumishi. Hii ni katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma.
Tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Corona
inapewa kipaumbele katika kipindi hiki. Tunatakiwa kuzingatia Miongozo
inayotolewa na Wizara ya Afya pamoja na maelekezo ya Viongozi Wakuu wa Nchi.
Aidha, watumishi wa umma na wananchi
wote wanataarifiwa kuwa wanaweza kuwasilisha kero na malalamiko yao kwa kutuma
kwa barua pepe kwa anuani ya secretary@psc.go.tz
au kupiga simu namba 0738 166 703.
Kupitia maadhimisho haya Tume inawakumbusha
Waajiri, Mamlaka za Ajira, Mamlaka za Nidhamu pamoja na Watumishi wa Umma kuhakikisha
wakati wote wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu,
Miongozo na Maelekezo halali yanayotolewa na Serikali.
Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Wiki ya
Utumishi wa Umma kwa mwaka 2020 ni: “Jukumu
la Utumishi wa Umma katika Kujenga na Kudumisha Amani iliyopo Miongoni mwa
Jamii”.
Imetolewa na:
Richard M.Cheyo
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Tume ya Utumishi wa Umma.
DAR ES SALAAM
16 Juni, 2020
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...