Na Amiri kilagalila,Njombe
Wafugaji wa samaki mkoani Njombe wametakiwa kuwekeza zaidi katika ufugaji huo kufuatia utafiti kuonyesha fursa kubwa ya zao  hilo kwa aina ya Kambale, Sato na Perege
Kwa muda mrefu wakazi wa mkoa wa Njombe wamekuwa hawafugi samaki katika baadhi ya maeneo kwa kuhofia hali ya hewa ya baridi ambapo Niko Msigwa mkulima wa kijiji cha Kinenulo ameanza kunufaika na ufugaji wa huo
Biashara ya samaki mkoani Njombe imekuwa na soko la ndani la uhakika na ndio sababu iliyo msukuma Msigwa kuanza ufugaji huku akikiri kupata faida kubwa.
“Soko la samaki sasa hivi linafanya vizuri yaani sasa hivi samaki aina ya Sato ni bei kubwa,ukienda hata sokoni pale kilo moja ni Sh.12,000 na wao wanajumua kilo moja Sh.7,000 mpaka 8,000”alisema Msigwa
Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Kinenulo wamezungumzia ufugaji na mahitaji ya samaki mkoani Njombe.
“Nilichojifunza mimi samaki wanafaa kwa matumizi ya binadamu lakini wanaongeza kipato,na wangejitokeza wengi kufuga ingekuwa vizuri kwasababu hata sisi hapa samaki wengi wanatoka Njombe”alisema Ephrahim Fungo mkazi wa Kinenulo
Samaki Ambao wapo Kwenye Kundi Muhimu la Mlo Kamili Kwa ajili ya Lishe Pia Wamekuwa Kitoweo Kizuri Kwa Watanzania Hatua Inayochagiza Jamii Kuona Umuhimu wa Kuwafuga Kibiashara.

Ufugaji wa Samaki ni neema Njombe

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...