Na Emmanuel J. Shilatu

Napenda niungane na Mamilioni ya Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Watanzania kwa ujumla kumpongeza Mwenyekiti CCM Taifa na Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuandika historia ya aina yake kwenye mkutano Mkuu wa CCM Taifa uliofanyika leo Julai 11, 2020 mjini Dodoma.

Kwanza, Dkt. Magufuli amethibitishwa kwa kupigwa kura ya ndio na Wajumbe 1822 wote sawa na asilimia 100 kupeperusha bendera ya CCM kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka huu utakaofanyika mwezi Oktoba, 2020.

Haijawahi kutokea katika historia ya miaka yote ndani ya CCM Mgombea kwa nafasi ya Urais kupitishwa kwa asilimia 100. Mwaka 2015 Dkt. Magufuli alipitishwa kwa asilimia 87. Ongezeko hili ni ishara ya kubaliko la uadilifu, uzalendo, ufuatiliaji, uchapa kazi, ukweli na ucha Mungu alionao Dk. Magufuli kiuongozi. 

Pili, Dk. Magufuli akiwa Mwenyekiti wa Kikao amewadhihirishia Watanzania na Dunia kwa ujumla juu ya Demokrasia iliyokomaa, uwazi na Uhuru wa uchaguzi ndani ya CCM kwa kura kupigwa wazi wazi na kuhesabiwa wazi wazi tena ikionyeshwa mubashara (live) na vyombo vya habari. Hii rekodi ameivunja na haijawahi kutokea katika historia ya Miaka yote ya chaguzi za CCM kwenye nafasi ya kumpata Mgombea Urais.

Hakika, Dk. Magufuli alivyosema uchaguzi wa mwaka huu atahakikisha unakuwa wa huru na haki alimaanisha na anaonyesha kivitendo kuanzia ndani nyumbani kwake (CCM).

Narudia tena kusema historia aliyoiandika Dkt.  Magufuli ni ya aina yake inayompambanua kivitendo kuwa Mwamba na mkufunzi wa Dunia juu ya siasa safi, Demokrasia ya kweli na Uhuru wa uchaguzi.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki CCM
Mungu Mbariki Dk. Magufuli

*Shilatu E.J*
0767488622

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...