mchimbaji mdogo wa Madini ya Tanzanite Bw. Saniniu Laiza akisaini kitabu mara baada ya kufika katika banda la GST katika maonesho ya 44 ya kibiashara katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
mchimbaji mdogo wa Madini ya Tanzanite Bw. Saniniu Laiza akiwa katika Picha ya pamoja
Na Samwel Mtuwa - DSM.
Leo Julai 12, 2020 , mchimbaji mdogo wa Madini ya Tanzanite, Saniniu Laiza ameipongeza Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kwa Utafiti za uhakika inazofanya katika sekta ya Madini nchini.
Laiza amesema hayo leo alipotembelea Banda la GST katika maonesho ya 44 ya Sabasaba yanayotarajiwa kufungwa kesho.
Akizungumza na Daktari Mussa Budeba ambaye ni Mtendaji Mkuu wa GST wakiwa katika banda hilo, mchimbaji Laiza aliwapongeza wataalam wa GST kwa juhudi kubwa wanazofanya kwa wachimbaji wadogo wa Madini kwa kuwaelekeza juu ya uchimbaji bora na wenye tija kwa uchumi.
Sambamba na pongezi hizo kwa GST Mchimbaji Laiza alipata fursa ya kupiga picha ya pamoja na wataalam ikiwa ni ishara ya kuonesha kuwa ametembelea Banda hilo.
Mapema baada ya kumaliza kuzungumza na mchimbaji Laiza, Dk. Budeba alizungumza na vyombo mbalimbali vya Habari juu ya majukumu ya GST
Mnamo Juni 24, 2020 Serikali kupitia Wizara ya Madini ilitangaza kupatikana kwa madini mawili ya Tanzanite moja likiwa na kilogram 9.2 na lingine likiwa na kilogram 5.8 yaliyochimbwa na Mchimbaji huyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...