Mkurugenzi wa Taasisi ya Haki za Wanawake (HAWA) Joyce Kiria akizungumza na Waaandishi wa Habari (Hawapo pichani ) wakati akitoa wito kwa wanawake kujitokeza katika kugombea nafasi mbalimbali wakati wa uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu.


Na Dixon Busagaga.

Mkurugenzi wa taasisi ya Haki za Wanawake (Hawa) Joyce Kiria amewataka wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi mkuu.

Amesema kwa mfumo ambao umetengenezwa sasa na serikali ya awamu ya tano, mchakato wa kugombea umeondolewa urasimu hivyo kutoa nafasi hata watu wasio na fedha kuwania na kuchaguliwa.

Kiria alisema endapo wanawake wengi watajitokeza na kuchaguliwa itasaidia utungwaji wa sera na sheria zitakazosaidia kukabiliana na changamoto zinazozikabili kundi hilo.

Alisema chini ya uongozi wa awamu ya tano jitihada kubwa zimefanyika kuhakikisha inaboresha sekta ya afya kwa kujenga vituo vya afya, dawa hatua iliyochangia kupunguza vifo vya wanawake na watoto.

“Ile dhana ya kwamba wanawake ni wapiga kampeni na kuwanadi wagombea tuachane nayo. Tujitokeze kwa wingi kugombea na kuchaguana. Rais John Magufuli ameondoa urasimu kabisa hivyo sasa hivi sio lazima uwe na fedha nyingi ndio upate nafasi ya kugombea. Ametutengenezea mazingira mazuri ya kuingia kwenye mchakato.

Twendeni tukagombee, tukachukua hizo nafasi ili tumsaidie rais ambaye ameonyesha jitihada kubwa katika kutukwamua wanawake. Amewaamini wanawake wengi na wamefanya kazi nzuri iliyotukuka,”

Kiria alisema uwepo wa wanawake wengi kwenye ngazi za maamuzi utasaidia utungwaji wa sheria na sera zitakazoondoa ukandamizaji wa kundi hilo na kuwakwamua katika nyanja mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...