Na Mwandishi wetu.

Benki ya Maendeleo TIB imeendelea kuhamasisha shughuli za uwekezaji katika Maonesho ya Wakulima ‘Nane Nane’ yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Maonesho Nyakabindi vilivyopo mjini Bariadi mkoani Simiyu.

Benki ya Maendeleo ya TIB na baadhi ya wateja wake wanashiriki maonesho hayo ili kutoa elimu kwa umma, kutangaza huduma inayozitoa pamoja na kuvutia wawekezaji kwa ajili ya uwekezaji wa kimkakati katika miradi mbalimbali hapa nchini.
Afisa Mwandamizi wa Masuala ya Bima wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. James Manyama (kushoto) akitoa elimu ya Bima ya Kilimo kwa mmoja wa wananchi waliotembelea Banda la TIB katika Viwanja vya Maonesho Nyakabindi vilivyopo mjini Bariadi mkoani Simiyu.
 Afisa Mwandamizi wa Usimamizi wa Miradi  wa Benki ya Maendeleo TIB, Bibi Mwajuma Milanzi (kushoto) akitoa maelezo ya Dirisha la Kilimo linalojihusisha na mikopo katika sekta ya kilimo  kwa mmoja wa wananchi waliotembelea Banda la TIB katika Viwanja vya Maonesho Nyakabindi vilivyopo mjini Bariadi mkoani Simiyu.
 Meneja Mauzo wa Kampuni ya AMIMZA, Bw. Mustafa Mohammed akitoa maelezo ya bidhaa zinazozalishwa na kampuni hiyo. Kampuni ya AMIMZA ni moja ya wateja wa Benki ya Maendeleo TIB waliopata fursa ya kutangaza bidhaa zao wakati wa   Maonesho ya Wakulima ‘Nane Nane’ yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Maonesho Nyakabindi vilivyopo mjini Bariadi mkoani Simiyu.
 Afisa Masoko wa Kampuni Matongo Farming Co. Limited, Bw. Clement Lissawa (kushoto) akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi aliotembelea Banda la TIB.
Mtaalamu wa Masuala wa Ufundi wa Kampuni ya Mwasonge, Bw. John Masero (kushoto) akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi aliotembelea Banda la TIB.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...