KATI ya wasichana 10 wanaofanya vizuri katika anga ya Muziki wa kizazi kipya alias bongofleva , huwezi kuacha kumtaja mwanadada Nandy.
Nandy ambae kwa Sasa amepata dili nyinyi na kuonekana miongoni mwa wasichana wenye maendeleo.
Nandy
ambae kwa sasa ni balozi wa makampuni mengi likiwemo kampuni ya nywele
aina Darling amesema pamoja na kipato chake lakini sio mtu wa majivuno na
kujiona super star.
Nandy
akizungumza na Michuzi TV wakati wa kutambulisha bidhaa mpya ya nywele
ya darling amesema anapenda maisha ya kujichanganya na watu tofauti
tofauti ili ajifunze vingi.
"Mara
nyingi nimekua mtu wa kula na mashabiki kwenye sehemu mbalimbali ila
huwa sio mtu wa kujionyesha Sana kiasi watu wanashindwa kujua Kama huwa
ni moja ya vitu ambavo napenda,"
Hata
hivyo wakati huo huo nandy aliwanunulia mashabiki zake mishikaki ya
shilingi elfu 25 na kuwagaia ikiwa ni sehemu ya kuonyesha kuwa
anayapenda maisha ya kula pamoja na shabiki zake
pia nandy amekanusha kuwa na ugomvi na Lulu diva.
"Ni maneno tu wala msiyafuatishe, Mimi ni shabiki wa Luludiva na Mara nyingi nasikiliza wimbo wake wa Gugugaga,"
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...