NA MWANDISHI WETU, SIMIYU

MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeanza rasmi kulipa Fao la Uzazi kwa wanachama wake wanawake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Angellah Kairuki ameelezwa hayo alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye maonesho ya Nanenane viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu Agosti 3, 2020.

Afisa Mkuu wa Mafao PSSSF, Bw. Daniel Dugilo amemueleza Mhe. Waziri kuwa PSSSF imeanza rasmi kulipa Mafao hayo ambayo yalisita kufuatia Serikali kuuunganisha mifuko minne ya Hifadhi ya Jamii ya PSPF, PPF, LAPF, na GEPF.

"Mhe. Waziri napenda pia niseme kuwa PSSSF imeanza rasmi kulipa fao la uzazi kwa wanachama wetu wanawake, itakumbukw akwamba ulipaji wa fao hili ulisitishwa kwa muda kutokana na kuunganishwa kwa mifuko." Alisema Dugilo.

Akifafanua zaidi kuhusu vigezo vinavyozingatiwa kulipa fao hilo, Kaimu Meneja wa PSSSF mkoa wa Mara, Bi.Nyaswi Elias alibainisha kuwa ni lazima mfaidika awe ni mwanachama wa PSSSF mwanamke aliyechangia kwa miezi 36 sawa na miaka mitatu (3) na anapaswa kuwasilisha nyaraka zote zinazohitajika kwenye mfuko ndani ya siku Tisini (90) baada ya kujifungua.

Masharti hayo alisema, “Fao hilo la uzazi mwanachama anaweza kufaidika nalo kwa uzao wa kwanza, wapili, watatu hadi wanne haijalishi katika moja ya uzao huo kajifungua mtoto mmoja au mapacha au kila uzao kajifungua mapacha, tunachozingatia hapa ni kwamba mwachama atafaidika na fao hilo mara mara nne.”
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Angellah Kairuki (wapili kushoto), akiwa na Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga(wakwanza kushoto), wakisikiliza maelezo kuhusu shughuli za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kutoka kwa Afisa Mkuu wa Mafao, PSSSF Bw.Daniel Dugilo (aliyeipa mgongo camera), wakati mawaziri hao walipotembelea banda la PSSSF kwenye viwanja vya Nyakabindi kunakofanyika maonesho ya Nanenane kitaifa Agosti 3, 2020.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Angellah Kairuki (w (kushoto), akiwa na Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga(katikati), wakisikiliza maelezo kuhusu shughuli za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kutoka kwa Afisa Mkuu wa Mafao, PSSSF Bw.Daniel Dugilo (aliyeipa mgongo camera), wakati mawaziri hao walipotembelea banda la PSSSF kwenye viwanja vya Nyakabindi kunakofanyika maonesho ya Nanenane kitaifa Agosti 3, 2020.
 Aliyekuwa Katibu Tawala mkoa wa Simiyu Jumanne Sagini (wapili kushoto) akifurahia jambo alipotembelea banda la mfuko huo Agosti 3, 2020.

 Kaimu Meneja wa PSSSF mkoa wa Mara, Bi.Nyaswi Elias 




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...