Mkuu wa Idara ya Mawasiliano Serikalini Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi. Dorina Makaya (wa pili kushoto) na Meneja Msaidizi Kanda ya Kati, Patricia Manonga ( wa tatu kulia), wakiwa na baadhi ya watumishi wa wizara hiyo, Taasisi na vyuo wakisherehekea ushindi walioupata baada ya kukabidhiwa cheti cha ushindi wa kwanza katika kundi la sekta ya uchumi na uzalishaji wakati wa kilele cha Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Kati kwenye viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia maswala ya Walemavu mhe. Stella Ikupa ( wa kwanza kulia) akimkabidi cheti kwa niaba ya Wizara ya Maliasili na Utalii Mkuu wa Idara ya Mawasiliano Serikalini Bi. Dorina Makaya (mwenye T-shirt nyeupe) na Bi. Patricia Manonga (wa kwanza kushoto) kwenye halfa ya kilele cha Maonesho ya Nane Nane jijini Dodoma.Attachments area
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano Serikalini Bi. Dorina Makaya (kulia) na Mratibu wa Maonesho ya Nane Nane (kushoto) wakiongoza wadau kuingia banda la wanyama kwenye Maonesho ya Nane Nane jijini Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...