******************************

Mkuu wa wilaya ya Arusha Mh Kenani Kihongosi leo ameanza ziara ya kikazi kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika Tarafa ya Elerai, katika Kata ya Murrieti ambapo amepokea kero mbali kutoka kwa wananchi na Kuzielekeza mamlaka husika kuzichukulia hatua na kero nyingine ameweza kuzitatua papo kwa papo, Mh kenani Amesema “Jukumu letu viongozi sio kukaa ofisini Bali ni kufika kwa wananchi wetu na Kuwatatulia kero zao, Mhehsimiwa Rais Dr John Pombe Magufuli halali sasa nitashangaa kuona watumishi mnalala badala ya kwenda Kuwasikiliza wananchi,hivyo mimi ni Mtumishi wenu wana Arusha na nitawatumikia kuhakikisha tunamaliza kero zenu” Katika ziara Hiyo mkuu wa wilaya Aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji pamoja na Wataalamu wa halmashauri ya Jiji la Arusha. Ziara ya Mkuu wa Wilaya itaendele kesho Tar 11.08.2020 katika Ofisi za kata ya Murrieti.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...