Waziri wa Madini Dotto Biteko aipongeza Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania  (GST) juu ya tafiti za jiosayansi inazofanya katika sekta ya Madini.

Waziri Biteko ametoa pongezi hizo alipofika katika Banda la GST lililopo katika maonesho ya Tatu ya Tekinolojia na Uwekezaji katika sekta ya Madini yanayoendelea mkoani Geita.
Akiwa katika Banda la GST na Mkuu wa Mkoa Geita Mhandisi Robert Gabriel waziri Biteko alisema kuwa Serikali inatambua mchango wa sekta ya Madini nchini na kushauri kuwa bidhaa za sekta ya Madini  zinazozalishwa nchini ziuzwe ili kufuata utaratibu wa Mpango ushirikishwaji kwa Wazawa katika sekta ya Madini  nchini.
Katika maonesho haya GST kupitia Idara  zake imemuonesha na kumuueleza mafanikio mbalimbali ikiwapo  vyungu maalum vya kuyeyushia dhahabu na akapendekeza ufanyike utaratibu wa kuuza vyungu hivyo katika mgodi wa dhahabu wa STAMIGOLD
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...