Majeneza yakiwa tayari yamepangwa Uwanjani wakati Ibada ya Kuombea Marehemu hao ikiendelea.
Sheikh wa Wilaya Karagwe Nassib Abdul akitoa nasaha zake wakati alipokuwa akisalimia waombolezaji
Sheikh wa Wilaya Kyerwa Sheikh Mrashani akiongoza Viongozi wa Dini katika Ibada Maalum Kuombea Marehemu wa Shule ya Byamungu.
Mmiliki wa Shule ya Byamungu Abdu Bushagama akitoa shukrani zake kwa Rais John Pombe Magufuli kwa kumtoa mahabusu baada ya kushikiliwa kufuatia Tukio la Ajali ya Moto.
Mzazi wa Marehemu Samweli Mohammed akisaidiwa na waombolezaji wengine kuelekea kwenye jeneza la Mwanae.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Taifa Dkt. Bashiru Ally akiongoza viongozi wengine kutoa Salaam kwa Marehemu Watoto wa Shule ya Msingi Byamungu.
Kwa Niaba ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali Katibu Mkuu wa CCM akitoa salaam za pole kwa waombolezaji
MIILI Kumi ya Watoto waliokuwa Wanafunzi wa Shule ya msingi ya Kiislamu ya Byamungu iliyopo Kyerwa imeagwa rasmi leo katika Viwanja vya Shule hiyo Mara baada ya shughuli ya utambuzi wa Vinasaba kukamilika.(Picha na Abdullatif Yunus, Michuzi TV.)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...