Na Amiri Kilagalila, Njombe
BAADHI ya wanawake mkoani Njombe wamesema wameshindwa kuwania nafasi za uongozi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu kutokana na kuzuiliwa na baadhi ya waume zao.

Wamesema nafasi ya mwanamke kwenye uongozi zimeendelea kupigiwa kelele kwaajili ya kutetea haki zao lakini wamekuwa wanahofia kuharibu ndoa na wengine wanazuiliwa na waume zao.

Nao baadhi ya wanaume mjini Njombe wamekili kutowaruhusu wake zao kuwania nafasi za uongozi kwa ngazi za ubunge na udiwani kwa kuhofia kuolewa na wanaume wengine na kusababisha ndoa kuvunjika.

Viongozi wa vyama vya siasa mkoani Njombe wamesema kuwa wametoa nafasi nyingi kwa wanawake kushiriki kuwania uongozi isipokuwa baadhi yao wamekuwa waoga kujitokeza.

Afisa ustawi wa jamii mkoa wa Njombe Teresia Yomo amesema,kwa sasa wanawake wanaonesha ushiriki mkubwa kuwania nafasi za uongozi na kwamba mwanamke akiwa kiongozi atatetea haki za wanawake wenzao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...