Kamishna wa Wanyamapori Kamishna Mabula Misingwi 

********************************* 

NA FARIDA SAIDY, MOROGORO. 

Mamlaka ya usimamizi wa Wanyamapori Nchini (TAWA) imeanzisha utaratibu wa kuuza nyama za wanyamapori kwenye Bucha zilizo chini ya Mamlaka hiyo ili kutoa fursa kwa kila Mwananchi aweze ya kutumia kitoweo hicho. 

Taarifa hiyo imetolewa na Kamishna wa Wanyamapori Kamishna Mabula Misingwi wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Mkoani morogoro ambapo amesema tangu kutolewa kwa agizo hilo wamekuwa wakifanya tahmini kuhusu taratibu utakao tumika kuuza nyama hizo. 

Hata hivyo ameendelea kusema kuwa katika kurudisha faida kwa wananchi TAWA imeanzisha miradi mbalimbali ukiwemo mradi wa ufugaji nyuki ambao unazalisha tani 1000 za asali na zaidi ya vikundi 58 na wanachama 268 wamenufaika na mradi huo. 

Katika hatua nyingine amesema ili kupunguza uvamizi unaofanywa na wanyamapori katika maeneo ya makazi na mshamba hapa nchini,amewashauri Wananchi kuishi katika maeneo yaliorasimishwa kwa makazi ili kujilinda na wanyama wakali na waharibifu wanaotoka katika mbuga za wanyama na hifadhi za Taifa. 

Hata hivyo amesema wanaendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kuthamini, kulinda na kudhibiti ujangili wa wanyamapori walio karibu na maeneo yao, ambapo mpaka sasa club 163 zimeanzishwa katika shule za msingi kwa lengo la kuwapatia elimu namna ya kuweza kuepukana na wanyama wakali na waharibifu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...