Mganga Mkuu wa Serikali Dkt.Abel Makubi akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa ASCEND unaolenga katika kuimarisha Tafiti za majaribio ya dawa pamoja na maadili ya tafiti za Afya nchini na kufuatilia usalama wa madhara yatokanayo na matimizi ya dawa. Taasisi zinazoshiriki katika mradi huu ni TMDA, NIMR, ZFDA, KCRI, MUHAS, ZAHRI na ST. Andrew's University ya Uingereza.  Mradi huu ambao ni wa miezi 30 utasaidia kujengea uwezo watafiti wachanga kwa kupata mafunzo mbalimbali toka MUHAS na kuimarisha mifumo ya tafiti mbalimbali za Afya nchini.    Uzinduzi huu umefanyika jijini Dar es Salaam tarehe 26 Novemba, 2020 chini ya  uratibu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Adam Fimbo akitoa maelezo kuhusiana na Mradi wa majaribio ya Dawa na Utafiti uliozinduliwa jijini Dar es Salaam.
Meneja Mawasiliano na Elimu kwa Umma,wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA),Gaudensia Simwanza  akitoa maelezo ya uzinduzi wa Mradi  uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Mganga Mkuu wa Serikali Dkt.Abel Makubi akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa  TMDA mara baada ya kuzindua mkutano wa Mradi wa Ascend jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya washiriki wa Taasisi mbalimbali wakiwa katika uzinduzi wa mkutano wa Mradi wa Ascend wa uboreshaji mifumo ya Udhibiti wa majaribio ya dawa taifiti mbalimbali na Udhibiti wa usalama wa dawa uliofanyika jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Emmanuel Massaka MMG.)


*Mganga Mkuu wa Serikali ataka gharama kwa wanafunzi watafiti zipungwe

*TMDA kutoa mafunzo kwa wadau kujenga uelewa 

Na Chalila Kibuda, Michuzi TV

SERIKALI imesema kuwa itatoa ushirikiano katika mradi wa Ascend unaolenga kuboresha mifumo ya udhibiti wa majaribio ya dawa,tafiti mbalimbali na udhibiti wa usalama wa dawa zitakazoleta tija kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Hayo ameyasema Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Abel Makubi wakati akizundua Mradi wa miaka miwili wa uboreshaji wa mifumo ya Udhibiti wa majaribio ya dawa ambao uko chini ya Mamlaka ya Dawa ,Vifaa Tiba (TMDA) uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Dkt. Makubi amesema katika uzinduzi wa mradi wa ASCEND unaolenga kuimarisha Tafiti za majaribio ya dawa pamoja na maadili ya tafiti za afya nchini na kufuatilia usalama wa madhara yatokanayo na matimizi ya dawa hayo.

Mradi huo ni unalenga kupunguza muda wa kutathmini maombi ya kufanya tafiti za majaribio ya dawa nchini na kuwezesha upatikanaji wa vibali vya utafiti kwa muda mfupi.

Taasisi zinazoshiriki katika mradi  ni Mamlaka ya Dawa,Vifaa Tiba (TMDA), Taasisi ya Taifa ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu  (NIMR,) Mamlaka ya  Chakula na Dawa Zanzibar(ZFDA,) KCRI, MUHAS, ZAHRI na ST. Andrew's University ya Uingereza pia mradi huo   ambao ni wa miezi 30 utasaidia kujengea uwezo watafiti wachanga kwa kupata mafunzo mbalimbali toka MUHAS na kuimarisha mifumo ya tafiti mbalimbali za Afya nchini.  

Dkt. Makubi ameiangiza TMDA kupunguza gharama  kwa wanafunzi wanaofanya Utafiti kwani wao ndio wanaotegemewa kuwa wataalam kuja kuhudumia taifa.

Aidha Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa ,Vifaa Tiba (TMDA) Adam Fimbo amesema  katika Mradi huo pia watatoa mafunzo katika Kituo cha Muhimbili ili kujenga uelewa mpana kwa Tanzania Bara na Zanzibar.

Amesema kuwa kupatikana kwa mradi huo wamepitia miongozo mbalimbali na kusaidia TMDA kupata ruzuku hizo katika mradi.

"Mradi huu utaleta matokeo chanya katika masuala ya majaribio ya tafiti za dawa na hivyo Taifa kunufaika katika maendeleo ya tafiti hizo ambapo nchi zingine zilishapata na zikaweza kupata mafanikio."amesema Fimbo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...