Na Woinde Shizza , Michuzi  Tv Arusha

JUMLA  ya  wanawake na watoto 2558 wamefanyiwa ukatili mkoani Arusha sawa na ongezeko la 22% kutoka mwaka 2918/2019 ambapo ukatili kwa watoto ulikuwa jumla 988.

Akizindua kampeni ya siku 16 za kuzuia  ukatili wa kijinsia  Jana mkuu wa mkoa wa Arusha Iddy Kimanta alisema  idadi imeongezeka kwa kiasi kikubwa mwaka huu ambapo kutoka idadi ya watoto 988 mwaka 2018/2019  idadi imepanda hadi kufikia  1256 kwa watoto.

"Mwaka huu idadi ni kubwa  naamini nikiendelea kuwepo mwakani tunatamani kuwa kati ya mikoa ambayo ina idadi ndogo au kutokuwepo kabisa kwa ukatili wa  wanawake na watoto" Alisema Kimanta.

Alisema tabia za  ukatili wa kijinsia zimekuwa zikiathiri na kupelekea madhara makubwa katika familia nyingi ambapo alisema wakina mama na baadhi ya kina baba wanaathiriwa na ukatili huu kutokana na watoto wao kufanyiwa vitendo hivyo.

Alitoa rai kwa wadau mbalimbali kuwajengea uwezo watoto wa kuweza kuripoti pindi wanapofanyiwa ukatili huu akidai kuwa watoto wanapofanyiwa hayo wanakosa ujasiri wakuweza kutoa taarifa na kubaki na maumivu ya moto kwa muda mrefu.

"Watoto wengine hulazimika kuacha shule, kukimbia katika familia zao,kupata ulemavu,wengine kujikuta ndoa za utotoni pamoja na viwango vya ufaulu kushuka lakini matukio yote haya yanatokea katika jamii zetu na baadhi ya jamii hunyamazia bila kutoa taarifa" alisema.

Alitoa maagizo ya kila mmoja katika nafasi yake kuhakikisha  wanachukua hatua kuweka mazingira salama, majumbani, kazini, shuleni na hata mitaani na kutoa taarifa dawati la jinsia pindi yanapotokea matukio ya ukatili.

Uzinduzi huo umefanyika mkoani Arusha huku ukiudhuriwa na taasisi mbalimbali zinashughulika na maswala ya unyanyasaji  wa kijinsia, wanafunzi wa shule mbalimbali za mkoani hapa, na kauli mbiu ya mwaka huu,  'Tupinge ukatili wa kijinsia  mabadiliko yanaanza na Mimi' 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...