Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv


SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) wamesema kwa sasa nchi ina uwezo wa kuongeza mapato baada ya shiriko hilo kusitisha mkataba wa ukaguzi wa magari na mawakala unaoisha mwezi Februari mwaka huu.

TBS wamesema kuanzia hivi karibuni, wataanza kukagua magari wenyewe hapa nchini baada ya mkataba wao na kampuni ya ukaguzi wa magari kufikia Tamati mwezi Febrruari.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa udhibiti wa Ubora (TBS) Lazaro Msasalaga amesema utaratibu wa ukaguzi wa magari kuanzia mwezi Februari utafanyika hapa nchini chini ya Shirika lao.

Amesema, TBS ilianza ukaguzi wa magari  mwaka 2002 , na waliingia mkataba na mawakala  na wakawa wanafanya ukaguzi kwa niaba ya serikali na walikua wanatoa vyeti vya ubora 

Amesema, Programu hii iliweza kusaidia katika kuleta magari yenye viwango vya kimataifa , sasa mawakala walikua wanaingia mkataba wa miaka 3 na sasa  unamalizia hivi karibuni na magari yote yataanza kukaguliwa nchini ambapo awali yalikuwa yanakaguliwa nje ya nchi.

Msasalaga amesema, kuna faida kubwa sana kwa nchi kwa sababu kukaguliwa magari hapa nchini kutapelekea nchi kuongeza mapato, kutoa ajira kwa watalaamu na pia kujenga uwezo kwa vijana.

"Kwa sasa tupo katika maandalizi ya kuweka sawa seti za vifaa vya ukaguzi ambapo jumla ya seti 12 zitafungwa katika yadi zilizopo na kufanikisha kwa suala hili litasaidia taifa katika kuongeza mapato,"

"Utaratibu huo utasaidia pia kutoa ajira kwa vijana na ujuzi kwani tunaamini wapo watanzania wamesomea masuala ya ufundi," amesema Msasalaga

Aidha amesema, ukaguzi huo wa magari utafanywa ndani ya nchi kwa sasa na itakapobainika gari haijakidhi viwango mmiliki wa gari hilo atalipia matengenezo ya gari hilo na kisha litakaguliwa tena.

"Watu wa forodha (clearing and forwading) watafanya utaratibu wa kawaida na ukishakamilika wataingia kwenye ukaguzi, hilo linakuwa la mwisho baada ya kumaliza taratibu za kiforodha,"

Aidha, ameongezea kuwa , gharama za ukaguzi kwa gari moja ni kiasi cha Shillingi 350,000 na serikali walikuwa wanakosa fedha hizo na kupata asilimia 30 ya fedha za ukaguzi zilizokuwa zinalipwa wamiliki wa magari.

Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora Shirika la Viwango Tanzania, Bw.Lazaro Msasalaga (katikati) akitoa ufafanuzi kuhusu ukaguzi wa magari yanayotoka nje ya ya nchi.Alipofanya mkutano na wanahabari leo Makao Makuu ya Shirika hilo Jijini Dar es Salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...