MBUNGE wa Jimbo la Arusha Mjini Mrisho Mashaka Gambo ameendelea na ziara yake mtaa kwa mtaa ya kusikiliza kero za wananchi wake na kuzitafutia ufumbuzi kwa kushirikiana na Mamlaka husika, ameyasema hayo wakati akitembelea Kata ya Baraa.
Akiwa katika ziara hiyo Mbunge amewaahidi wananchi wa Kata hiyo kuwa atakuwa mstari wa mbele na kutumia nguvu kubwa kuhakikisha barabara ya Barakuda Soreni ambayo imekuwa kero sana kwa wakazi wa mtaa huo nakusababishia kukosa baadhi ya huduma za kijamiii inatengenezwa na mamlaka husika.
Gambo ameendelea kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi wa Jimbo la Arusha pamoja na kueleza mambo makubwa ambayo yamefanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais DR. John Pombe Joseph Magufuli tangu achaguliwe mwaka 2015.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...