****************************************
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MAHAKAMA ya Wilaya ya Bagamoyo ,mkoani Pwani imewahukumu wahamiaji haramu 83 kwenda jela miaka miwili kwa tuhuma za kuingia nchini bila vibali ikiwa ni kinyume cha sheria.
Aidha , raia wa Tanzania wawili wamehukumiwa miaka 20 jela kwa tuhuma za kukutwa wakiwa wamewahifadhi wahamiaji haramu hao.
Katika hukumu iliyotolewa na Hakimu Mkazi Mahakama ya Wilaya ya Bagamoyo Mwanakombo Mmanya,ilisema  raia wa Ethiopia 81,Somalia mmoja na Malawi mmoja wamehukumiwa kwenda jela miaka miwili au kulipa faini Shilingi 500,000 kila mmoja.
Awali mwendesha mashitaka wa Idara ya Uhamiaji ,Mkoa wa Pwani Fadhili Festo alisema kuwa  wahamiaji haramu hao walikamatwa mwezi Januari na Februari mwaka huu katika maeneo tofauti ya Wilaya ya Bagamoyo.
Hata hivyo ,Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Mwanakombo Mmanya alimhukumu Julius Shija mkazi wa Makurunge Bagamoyo miaka 20 jela au kulipa faini ya Shilingi Milion 20  ikiwa ni baada ya kesi yake ya kukutwa na hatia ya  kuwahifadhi wahamiaji haramu 16 nyumbani kwake.
Mwingine aliyehukumiwa ni Eliah Lekule mkazi wa Arusha ambaye alihukumiwa miaka mitatu jela baada ya kukutwa na hatia akiwasindikiza  wahamiaji haramu wawili katika stendi ya mabasi ya Bagamoyo kuelekea Mkoa wa Dar es Salam.
Kufutia hukumu hiyo, Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Pwani Paul Eranga aliwaonya wamiliki wa mabasi wanaotumika kuwasafirisha wahamiaji haramu.
“Kwasasa wahamiaji haramu wanaopita katika Mkoa huu wamebadilisha njia ambazo walikua wakitumia awali za kupanda boti na bodaboda badala yake sasa wanasafirisha kwa mabasi ya abiria” anasema.
Alieleza ,basi lolote litakalokamatwa likiwa limebeba wahamiaji haramu baada ya kesi kumalizika litataifishwa na kuwa mali ya Serikali.
Eranga pia aliwaonya raia wa Tanzania ambao wamekuwa na tabia ya kuwahifadhi na kuwasaidia wahamiaji haramu kuvuka hapa nchini kuacha mara moja biashara hiyo kwani kwa atakayekutwa na hatia hatua za kisheria zitachukiwa kama onyo kwa wengine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...