Leo Ijumaa Machi 05, 2021 moto mkubwa ambao chanzo chake hakikufahamika mara moja, umeteketeza bar maarufu ya La Chaz Pub iliyopo eneo la Sinza Mori Manispaa ya Kinondoni, Dar es salaam.

Moto huo ulianza majira ya saa 9 alasiri uliteketeza eneo kubwa na bar hiyo kabla ya Jeshi la zimamoto na uokoaji kufika na kufanikiwa kuzima moto huo.

Akielezea chanzo cha moto Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji jijini Ilala, Ndg. Elimino Shang'a  amesema chanzo cha moto huo bado hakijafahamika na wanaendelea na uchunguzi, kuhusu thamani ya vitu vilivyoungua, taarifa rasmi itatolewa baadae. Picha na SamTiger, MichuziTV

Endelea kufuatilia Michuzi TV Updates kwa taarifa za papo hapo.

Sehemu ya La Chaaz Pub inavyoonekana sasa baada ya kuteketea kwa moto huo.

Askari Polisi wakiendelea kusimamia ulinzi eneo la tukio.



 







#ChaguaKupambana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...