Na Mwandishi wetu, Babati
WAKALA
wa barabara (TANROADS) Mkoani Manyara imejipanga kutekeleza matengenezo
ya kilomita 1,869.2 za barabara na madaraja 130 kwa makisio ya sh15.3
bilioni kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022.
Meneja
wa TANROADS Mkoani Manyara, mhandisi Bashiri Rwesingisa ameyasema hayo
mjini Babati kwenye kikao cha bodi ya barabara ya mkoa huo.
Mhandisi
Rwesingisa amesema kwa upande wa barabara zinazosimamiwa na TANROADS
mkoani Manyara, miradi 20 ya maendeleo ya gharama ya sh4.8 bilioni
itatekelezwa.
"Miradi 17
ya ukarabati kwa makisio ya sh3.7 bilioni na miradi sita ya upembuzi
yakinifu na usanifu wa kina na mradi mmoja wa usanifu ya sh1.1 bilioni,"
amesema mhandisi Rwesingisa.
Amesema
kazi nyingine ni kuendeleza usimikaji taa za barabarani, ujenzi wa
madaraja ya Bisgeta barabara ya Mogitu-Haydom na kukamilisha daraja la
Chubi barabara ya Singe-Sukuro.
"Pia
kuna madaraja mawili ya barabara ya Mirerani-Landanai, daraja la Sunya
barabara ya Kijungu-Sunya-Dongo na ujenzi na ukarabati wa kilomita 9.3
kwa kiwango cha lami," amesema mhandisi Rwesingisa.
Mkuu wa mkoa wa Manyara, Joseph Mkirikiti amewataka viongozi watimize wajibu wao katika suala zima la utunzaji wa barabara.
"Pamoja
na hayo tuhakikishe kuwa barabara zinatengenezwa na kutunzwa ili
zitumike na hasa wananchi wa hali ya chini wakiwemo wakulima
wanaosafirisha mazao yao kutoka shambani," amesema Mkirikiti.
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul alisema baadhi ya barabara za
pembezoni za mjini Babati zinapaswa kukarabatiwa ili ziweze kupitika kwa
muda wote.
Naibu Waziri
Gekul alisema pia suala la ujenzi wa uwanja wa ndege wa mkoa huo
linapaswa kupewa kipaumbele ili ujenzi wake uanze mara moja.
Mbunge
wa Jimbo la Hanang' mhandisi Samwel Hhayuma amesema ahadi ya kujengwa
kwa barabara ya lami Katesh hadi Haydom inapaswa kutekelezwa na pia
barabara za michepuko ziingizwe kwenye mpango wa ujenzi.
Mbunge
wa Jimbo la Kiteto, wakili msomi Edward Ole Lekaita ameeleza kuwa
daraja kwenye kata ya Sunya limesababisha changamoto ya kupitika pindi
wananchi wakitaka kuelekea kupata huduma ya matibabu katika kituo cha
Sunya na pia barabara zilizopo kwenye ilani kutoka Arusha kwenda Dodoma
kupitia Kiteto isitafsiriwe kuwa ni nyingi.
Mbunge
wa jimbo la Mbulu mjini, Paul Isaay amesema wakulima wanapata wakati
mgumu pindi wakitaka kutoa mazao mashamba kwani vibao vya kuruhusu
uzito wa magari ni tani tatu pekee kwenye baadhi ya maeneo.
Mbunge
wa jimbo la Mbulu vijijini Flatei Massay amesema maneno ya mchakato,
upembuzi yakinifu na usanifu yanapaswa kutekelezwa kwa vitendo ili
ujenzi wa barabara ya lami ya Karatu, Mbulu, Haydom, Singida uanze.
Mbunge
wa viti maalumu Regina Ndege amesema wanapaswa kushirikiana kati ya
wabunge na vitongozi wengine ili kuhakikisha barabara zilizoahidiwa
kwenye ilani ya uchaguzi zinatekelezwa.
Mbunge
wa Vijana Taifa, Asia Halamga amesema baadhi ya wanaosafisha mazingira
ya barabara kwenye wilaya ya Kiteto hawakuwalipa kwa wakati vijana
wanaosafisha barabara hivyo ikawalazimu yeye na mbunge wa Jimbo hilo Ole
Lekaita wawape fedha hizo.
Mkazi
wa Mjini Babati, Anaufoo Ulomi amesema visima vya maji vinapaswa
kuchimbwa pembeni ya barabara ili majanga yakitolea maji yapatikane kwa
urahisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...